Monday, March 25, 2013

BAADA YA KAJALA KUACHIWA HURU, HALI ILIKUWA HIVI NJE YA MAHAKAMA YA KISUTU.


Wema Sepetu leo amejizolea umaarufu wa kutosha baada ya kutoa mfukoni mwake shilingi milioni 13 kulipa faini aliyopigwa muigizaji mwenzie Kajala Masanja ambaye hukumu yake ilikuwa imetolewa  kwenda jela miaka mitano ama kulipa kiasi hicho cha fedha.
Kajala na Wema wakikumbatianaKajala na Wema wakikumbatiana
Akiongea  kwa  kujiamini, Wema amesema hakufikiria mara mbili kutoa kiasi hicho cha fedha.

“Kusema kweli wanasemaga kwamba kutoa ni moyo so naamini what I did is best, nimetoa kwasababu I had to do it and sikuthink twice kuhusu kufanya hivyo,”
 amesema Wema.
Wema akwa na KajalaWema akiwa na Kajala
 
“Nimefanya kama namsaidia rafiki yangu, ndugu yangu na sidhani kama ingekuwa ni kitu kizuri kumuona mwenzako anaingia kwenye dhahama, kwenye tabu, kwenye mateso na wakati nina uwezo wa kumsaidia kwahiyo I just did what I had to do.”

Kuachiwa kwa Kajala kumepokelewa kwa furaha kubwa na mastaa mbalimbali nchini.


Kajala akikumbatiana na ZamaradiKajala akikumbatiana na Zamaradi

No comments:

Zilizosomwa zaidi