Monday, March 25, 2013

WANAWAKE NA CHANGAMOTO YA KUMILIKI ARDHI....!

Naibu waziri wa katiba na sheria Bi. Angela Kairuki amesema richa
ya kuwa wanawake wamepewa fursa za wazi kabisa kisheria katika
kumiliki ardhi, bado umiliki wa ardhi ni mdogo sana nchini.

Kauli hiyo imetolewa leo wakati wa semina  ya Chama Cha Wanawake
 nchini (TAWLA) juu ya umiliki wa ardhi kwa wanawake na uwekezaji
 iliyofanyika jijini Dar es salaam.

Naibu waziri huyo amesema kutokana na muamko mdogo wa wanawake
kumiliki ardhi kwa kiasi cha juu, ndio kunawafanya washindwe kutumia
fursa za kisheria za kumiliki ardhi.

No comments:

Zilizosomwa zaidi