Sunday, January 20, 2013

MVUA KALI YASABABISHA MAFURIKO MJINI MTWARA

Mvua kubwa iliyonyesha mapema leo mjini Mtwara imepelekea mafuriko katika maeneo mbali mbali ya mji huu na kufanya wakazi wa maeneo haya kupata kuanza kuhangaika kuhamisha vitu vyao na wengine wakiwa hawajui la kufanya maana maji yamejaa mpakamajumbani mwao.

Ni balaa kubwa hasa eneo la Chuno Eneo hili ni karibu na nyumba ya Mzee Hokororo au Dr Mwakipa. Hali ni mbaya sana na maji yanaendelea kujaa hadi mchana huu.Hakuna taarifa yeyote mtu yeyote aliyepoteza maisha. Msaada wa haraka unahitajika kwa wananchi hawa.
 Picha na Mdau Abdulaziz

No comments:

Zilizosomwa zaidi