Monday, September 17, 2012

Wakazi wa kijiji cha Kwadelo kilichopo wilayani Kondoa mkoani Dodomg walalamika kwa kukosa huduma ya maji. Richa ya kuwa Mkoa huo una asili ya ukame, serikali imewaacha solemba wakazi wa kijiji hicho kwani hata visima havijachimbwa kijijini hapo. Akiongea mkazi wa kijiji hicho ambaye jina lake halikutajwa amesema, inawalazimu wanawake kutembea umbali mrefu usikt wa manane kutafuta maji jambo ambalo ni hatari kwa maisha yao. Serikali ikishirikiana na wakazi wa Kwadelo imeombwa kulishughulikia tatizo hili mapema kwani wamekuwa wakipata shida hiyo kwa mda mrefu.

No comments:

Zilizosomwa zaidi