Saturday, May 31, 2014

PETER MUTHARIKA AAPISHWA KUWA RAIS WA MALAWI

Hatimaye kiongozi wa upinzani wa Malawi Peter Muatharika leo ameapishwa kuwa rais mpya wa nchi hiyo baada ya Joyce Banda kushindwa katika uchaguzi wa rais uliokuwa na hali ya sitofahamu.
Rais huyo aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi na kaka wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo aliyefariki dunia Bingu Wa Muatharika, amekula kiapo leo mbele ya mahakama kuu ya nchi hiyo katika mji wa Blantyre. 
Katika hotuba yake ya kwanza baada ya kuapishwa, Peter Mutharika amekiri kuwa Malawi inakabiliwa na matatizo, lakini akataka washirikiane pamoja ili kuijenga nchi hiyo ambayo inaelekea kuanguka. Rais anayeachia ngazi Joyce Banda aliyeshindwa katika uchaguzi, hatimaye mapema leo alikubali matokeo na kumpongeza Mutharika kwa kushinda.  Baada ya uchaguzi Bi. Banda alidai kumetokea uchakachuaji na kuamuru uchaguzi ufutwe, suala ambalo halikuafikiwa na mahakama kuu ya Malawi.

No comments:

Zilizosomwa zaidi