Saturday, January 12, 2013

AZAM KULITWAA KOMBE LA MAPINDUZI KWA MARA NYINGINE


Azam FC yatwaa kwa mara ya pili Kombe la Mapinduzi  

Goli la mshambuliaji Gaudence Mwaikimba wa Azam FC limeipa ubingwa wa Kombe la Mapinduzi kwa mara ya pili mfululizo timu hiyo katika mchezo wa fainali ulimalizika kwa Azam FC kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Tusker FC ya Kenya.

Azam FC imeweza kutetea kombe hilo na kilibakisha nchini katika mchezo ulitumia dakika 120 kumalizika kwenye Uwanja wa Amaan, visiwani Zanzibar.

Mabingwa hao kwa mara ya pili walipewa medali za dhahabu, kombe na kitita cha shilingi milioni kumi kama zawadi ya kutwaa ubingwa huo.

Katika mchezo huo kipindi cha kwanza kilimalizika kwa timu zote bila kufungana, kipindi cha pili Tusker walianza kupata bao kupitia kwa mchezaji Jese Were aliyetumia uzembe wa beki ya Azam FC katika dakika ya 59.

Azam FC kupitia kwa beki wake mpya Jockins Atudo alisawazisha goli hilo kwa mkwaju wa penati baada ya mchezaji wa Tusker Luke Ochieng kunawa mpira wakati akizui mpira wa kichwa uliopigwa na Mwaikimba, penati ilimriwa na mwamuzi Ramadhan Kibo.

Goli hilo la kusawazisha kwa Atudo, ni goli lake la nne katika mashindano hayo, akifuatiwa na Mwaikimba mwenye magoli mawili.

Matokeo ya sare ya 1-1 yalimaliza dakika 90, katika dakika za nyongeza Mwaikimba alitumia vema nafasi aliyoipata katika dakika ya 92 na kupachika goli hilo wavuni na kumaliza mchezo Azam FC ikitwaa ubingwa kwa ushindi wa 2-1.

Baada ya goli hilo Azam FC walituliza mpira chini na kucheza mtindo wa kulinda lango lao kwa muda wote wa dakika 28 zilizobaki.

Katika mchezo wa leo Azam FC walifanya mabadiliko mawili, walitoka Uhuru Seleman dk 64 nafasi yake ikachukuliwa na Abdalah Seif na dk 126 aliingia Malika Ndeule kuchukua nafasi ya Brian Umony.

Tusker walifanya mabadiliko walitoka Fredrick Onyango, Andrew Tololwa, Jese Were, Khalid Aucho na Ismail Dunga nafasi zao zikachukuliwa na Mark Odhiambo, Edwin Ombasa, Andrew Sekayambya, Benson Amianda na Michael Olunga.

Baada ya kutwaa Kombe hilo, kocha mkuu wa Azam FC amewapongeza wachezaji wake kwa kubakisha kombe hilo na kusema ni muendelezo wa mipango ya mafanikio katika klabu hiyo.

Amesema safari inaendelea ya kupeleka makombe katika klabu hiyo, walianza na Mapinduzi 2012, Ngao ya Hisani walilochukua nchini Congo DRC na hili la Mapinduzi 2013.

Kikosi cha Azam FC kilichotwaa ubingwa, Mwadini Ally, Himid Mao, Samih Haji Nuhu, David Mwantika, Jockins Atudo, Michael Bolou, Humprey Mieno, Khamis Mcha, Gaudence Mwaikimba, Uhuru Seleman/Seif Abdalah 64’ na Brian Umony/Malika Ndeule 126’.

Wengine waliokuwa na kikosi hicho, Aishi Salum, Wandwi Wiliam, Luckson Kakolaki, Omary Mtaki, Abdi Kassim ‘Babi’, Jabir Aziz, Ibrahim Mwaipopo,Salum Abubakar, Tchetche Kipre kabla ya kuumia,  waliokosa mashidano hayo ni Abdulhalim Humud, John Bocco, Waziri Salum ambao ni majeruhi.Azam FC yatwaa kwa mara ya pili Kombe la Mapinduzi



Azam FC imeweza kutetea kombe hilo na kulibakisha nchini katika mchezo ulitumia dakika 120 kumalizika kwenye Uwanja wa Amaan, visiwani Zanzibar.
Goli la mshambuliaji Gaudence Mwaikimba wa Azam FC ndilo limeipatia ubingwa wa Kombe la Mapinduzi kwa mara ya pili mfululizo katika mchezo  ulimalizika kwa Azam FC kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Tusker FC ya Kenya.

Mabingwa hao kwa mara ya pili walipewa medali za dhahabu, kombe na kitita cha shilingi milioni kumi kama zawadi ya kutwaa ubingwa huo.

Katika mchezo huo kipindi cha kwanza kilimalizika kwa timu zote bila kufungana, kipindi cha pili Tusker walianza kupata bao kupitia kwa mchezaji Jese Were aliyetumia uzembe wa beki ya Azam FC katika dakika ya 59.

Azam FC kupitia kwa beki wake mpya Jockins Atudo alisawazisha goli hilo kwa mkwaju wa penati baada ya mchezaji wa Tusker Luke Ochieng kunawa mpira wakati akizui mpira wa kichwa uliopigwa na Mwaikimba, penati ilimriwa na mwamuzi Ramadhan Kibo.

Goli hilo la kusawazisha kwa Atudo, ni goli lake la nne katika mashindano hayo, akifuatiwa na Mwaikimba mwenye magoli mawili.

Matokeo ya sare ya 1-1 yalimaliza dakika 90, katika dakika za nyongeza Mwaikimba alitumia vema nafasi aliyoipata katika dakika ya 92 na kupachika goli hilo wavuni na kumaliza mchezo Azam FC ikitwaa ubingwa kwa ushindi wa 2-1.

Baada ya goli hilo Azam FC walituliza mpira chini na kucheza mtindo wa kulinda lango lao kwa muda wote wa dakika 28 zilizobaki.

Katika mchezo wa leo Azam FC walifanya mabadiliko mawili, walitoka Uhuru Seleman dk 64 nafasi yake ikachukuliwa na Abdalah Seif na dk 126 aliingia Malika Ndeule kuchukua nafasi ya Brian Umony.

Tusker walifanya mabadiliko walitoka Fredrick Onyango, Andrew Tololwa, Jese Were, Khalid Aucho na Ismail Dunga nafasi zao zikachukuliwa na Mark Odhiambo, Edwin Ombasa, Andrew Sekayambya, Benson Amianda na Michael Olunga.

Baada ya kutwaa Kombe hilo, kocha mkuu wa Azam FC amewapongeza wachezaji wake kwa kubakisha kombe hilo na kusema ni muendelezo wa mipango ya mafanikio katika klabu hiyo.

Amesema safari inaendelea ya kupeleka makombe katika klabu hiyo, walianza na Mapinduzi 2012, Ngao ya Hisani walilochukua nchini Congo DRC na hili la Mapinduzi 2013.

Kikosi cha Azam FC kilichotwaa ubingwa, Mwadini Ally, Himid Mao, Samih Haji Nuhu, David Mwantika, Jockins Atudo, Michael Bolou, Humprey Mieno, Khamis Mcha, Gaudence Mwaikimba, Uhuru Seleman/Seif Abdalah 64’ na Brian Umony/Malika Ndeule 126’.

Wengine waliokuwa na kikosi hicho, Aishi Salum, Wandwi Wiliam, Luckson Kakolaki, Omary Mtaki, Abdi Kassim ‘Babi’, Jabir Aziz, Ibrahim Mwaipopo,Salum Abubakar, Tchetche Kipre kabla ya kuumia, waliokosa mashidano hayo ni Abdulhalim Humud, John Bocco, Waziri Salum ambao ni majeruhi.

No comments:

Zilizosomwa zaidi