Wednesday, April 16, 2014

ATLECTICO MADRID KUMALIZA UTAWALA WA VIGOGO LIGI YA MABINGWA ULAYA?


NA GODFREY  MBAI
Hatua ya robo fainali ya ligi ya Mabingwa Barani Ulaya ilifikia tamati juma lililopita kwa timu nne kufanikiwa kufuzu hatua inayofuata ya nusu ya michuano hiyo ambayo fainali yake itapigwa katika jiji la Lisbon,Ureno.

Timu  nne zilizopata nafasi ya kucheza hatua ya nusu fainali msimu huu ni Atletico de Madrid(Spain),Real Madrid(Spain),Bayern Munich(German) na Chelsea(England).Kati ya timu hizo nne timu ya Atletico Madrid haikupewa nafasi kubwa ya kuweza kufika  katika hatua muhimu kama ya nusu fainali msimu huu kwa kuwa imekua na rekodi mbaya katika michuano hiyo.

Lakini kwa weredi wa kocha wa timu hiyo,Muargentina Diego Simeone na uwezo wa wachezaji wa timu hiyo,Atlectico Madrid sasa ipo mguu mmoja kuelekea nchini Ureno kucheza fainali ya ligi ya mabingwa baada ya kuwatupa nje ya mashindano wahispania wenzao,Barcelona katika hatua ya robo fainali katikati ya wiki iliyopita kwa ushindi wa jumla ya magoli 2-1 baada ya kucheza mechi mbili.

Ni wapenda soka wachache ulimwenguni walioipa nafasi ya kufika mbali,huku wengi wakiami kuwa ingeishia katika hatua za makundi au mikononi mwa Barcelona baada ya ratiba kuonyesha kuwa watacheza nao katika hatua ya robo fainali.Kwa mujibu wa ratiba ya hatua ya nusu fainali iliyotolewa na UEFA ijumaa iliyopita,Atlectico Madrid watacheza na Chelsea katika hatua hiyo.

Kinachofanya mpaka kujiuliza,kuwa Atlectico Madrid iliyoanzishwa 1903 kuwa wanaweza kuchukua ubingwa wa Ulaya msimu huu ni kwa kuwa rekodi zinaonyesha kuwa kuanzia bingwa wa msimu wa 2006/2007 mpaka 2012/2013 wote waliifunga Barcelona katika hatua tofauti tofauti katika msimu ambao Barcelona hawakuwa mabingwa  katika michuano hiyo yenye thamani kubwa duniani baada ya kombe la FIFA la dunia

Barcelona ilifungwa na Ac Milan katika hatua ya nusu fainali msimu wa 2006/2007 na kufanikiwa kutwaa taji baada ya kuwafunga Liverpool 2-1 katika fainali,mjini Athens,Ugiriki na msimu wa 2007,2008 Manchester United walichukua taji baada ya kuwafunga Chelsea mjini Moscow,Urusi kwa mikwaju ya penati na katika hatua ya nusu fainali waliwafunga Barcelona 1-0 Old Trafford kwa mkwaju wa mbali wa kiungo Paul Schooles,mechi ya kwanza iliisha  0-0.

2009/2010 Inter Milan ilikua bingwa baada ya kuwafungwa Buyern Munich 2-0 katika dimba la Santiago Bernebeu,Spainlakini nao katika hatua ya nusu fainali waliwafunga Barcelona enzi hizo Inter wakiwa chini ya kocha Jose Mourihno. 2011/2012 Chelsea ilichukua ndoo baada ya kuwafunga Bayern Munich katika fainali iliyoamuliwa kwa mikwaju ya penati baada ta kwenda 1-1 katika dimba la Allianz Arena,Ujereumani.

2012.2013 ubingwa ulikwenda Ujerumani ambapo timu ya Bayern Munich ilibeba kombe baada ya kuwafunga Wajerumani wenzao,Borrussia Dortmund 2-0 katika fainali iliyopigwa katika uwanja wa Wembley,England.

Hivyo swali linabaki,je msimu huu Atletico Madrid wataweza kufanya kile kilichofanywa na wengine kwa  kuchukua ubingwa wa ulaya kupitia mgongo wa Barcelona baada ya kuwafunga na kuwatupa nje ya michuano hiyo katika hatua tofautit tofauti?

Nafasi ya Atletico kuweza kufanya hivyo ipo na hii inatokana na jinsi timu hii ilivyojipanga msimu huu na  hii inaonekana kwa jinsi wanavyocheza kwa nidhamu kubwa katika mechi zao mbalimbali na licha ya kuwa katika hatua ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa msimu huu,pia kikosi hicho chenye nyota kama Diego Costa,Koke,Joao Miranda na wengine wengi ,kipo katika mbio za kuwania ubingwa wa Spain dhidi ya Barcelona na Real Madrid.

Hivyo muhimu ni kusubiri na kuona nini kitatokea kwa Atletico de Madrid msimu huu? Hatua ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa ulaya itachezwa April 22 na 23 kwa Atletico Madrid kucheza na Chelsea wakati Bayern watawavaa Real Madrid, huku mechi za marudiano ni wiki inayofuata.

No comments:

Zilizosomwa zaidi