VURUGU
na mizengwe vimeendelea kuandama uchaguzi ndani ya CCM, baada ya Katibu
wa CCM mkoani Arusha, Mary Chatanda kunusurika kupigwa katika uchaguzi
wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).
Katibu huyo alinusurika kipigo baada ya kutuhumiwa kutaka kuuvuruga uchaguzi huo wa kumpata mwenyekiti wa vijana mkoa.
Baadhi
ya wajumbe wa mkutano huo walimtuhumu Chatanda kuwa alitaka kuuvuruga
ili ampitishe mgombea ambaye ni chaguo lake aliyetajwa kwa jina la Dk
Harold Adamson.
Katika vurugu hizo, Chatanda
alinusurika kupigwa na wajumbe waliotoka Wilaya ya Monduli ambao
walitaka uchaguzi urudiwe ili haki itendeke.
Dalili za
kuibuka kwa vurugu zilianza kujitokeza mapema baada ya makundi ya
baadhi ya vigogo wa CCM yanayohusishwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward
Lowassa na Waziri wa Mambo ya Nje, Bernad Membe kutambiana nje ya ukumbi
wa mkutano.
| |
Wednesday, October 10, 2012
Uchaguzi UVCCM Arusha ni vurugu tupu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
Msanii maarufu wa Hip...
-
Arsenal v/s Tottenham Hotspur Liverpool v/s Wigan Athletic Manchester City v/s Aston Villa Newcastle United v/s Swansea City Queens Par...
-
Uhuru Kenyatta REPLY To Raila Odinga 1.The constitution does not impose any duty On IEBC to register voters, identify voters or tra...
-
Maelfu ya waathiriwa wanapokea matibabu baada ya vijiji vyao kuathirika kutokana na madini yenye sumu ya Lead na sumu inayotokana na migo...
-
Serikali ya Nigeria inasema kuwa iko tayari kuzingatia mbinu zote zitakazowezesha kuac...
No comments:
Post a Comment