|
VURUGU
na mizengwe vimeendelea kuandama uchaguzi ndani ya CCM, baada ya Katibu
wa CCM mkoani Arusha, Mary Chatanda kunusurika kupigwa katika uchaguzi
wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).
Katibu huyo alinusurika kipigo baada ya kutuhumiwa kutaka kuuvuruga uchaguzi huo wa kumpata mwenyekiti wa vijana mkoa.
Baadhi
ya wajumbe wa mkutano huo walimtuhumu Chatanda kuwa alitaka kuuvuruga
ili ampitishe mgombea ambaye ni chaguo lake aliyetajwa kwa jina la Dk
Harold Adamson.
Katika vurugu hizo, Chatanda
alinusurika kupigwa na wajumbe waliotoka Wilaya ya Monduli ambao
walitaka uchaguzi urudiwe ili haki itendeke.
Dalili za
kuibuka kwa vurugu zilianza kujitokeza mapema baada ya makundi ya
baadhi ya vigogo wa CCM yanayohusishwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward
Lowassa na Waziri wa Mambo ya Nje, Bernad Membe kutambiana nje ya ukumbi
wa mkutano.
| |
Wednesday, October 10, 2012
Uchaguzi UVCCM Arusha ni vurugu tupu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
Israel Magesa Wakili Magesa aliyeko (pichani) amefariki dunia ghafla leo asubuhi. Wakili Magesa, ambaye ni mmiliki wa kampuni y...
-
GARI aina ya Toyota VX linaloelezwa kuwa mali ya Serikali limekamatwa na polisi likiwa limebeba pembe za ndovu. ...
-
-
Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemkamata mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji likimtuhumu kuchochea vurugu za kupinga mradi wa bo...
-
Nimepokea mwaliko wa kikao maalumu cha kikao cha fedha na uongozi wa tarehe 3/01/2014 kikao kufanyika tarehe 06/01/2013 saa nane mchana ...
No comments:
Post a Comment