|
VURUGU
na mizengwe vimeendelea kuandama uchaguzi ndani ya CCM, baada ya Katibu
wa CCM mkoani Arusha, Mary Chatanda kunusurika kupigwa katika uchaguzi
wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).
Katibu huyo alinusurika kipigo baada ya kutuhumiwa kutaka kuuvuruga uchaguzi huo wa kumpata mwenyekiti wa vijana mkoa.
Baadhi
ya wajumbe wa mkutano huo walimtuhumu Chatanda kuwa alitaka kuuvuruga
ili ampitishe mgombea ambaye ni chaguo lake aliyetajwa kwa jina la Dk
Harold Adamson.
Katika vurugu hizo, Chatanda
alinusurika kupigwa na wajumbe waliotoka Wilaya ya Monduli ambao
walitaka uchaguzi urudiwe ili haki itendeke.
Dalili za
kuibuka kwa vurugu zilianza kujitokeza mapema baada ya makundi ya
baadhi ya vigogo wa CCM yanayohusishwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward
Lowassa na Waziri wa Mambo ya Nje, Bernad Membe kutambiana nje ya ukumbi
wa mkutano.
| |
Wednesday, October 10, 2012
Uchaguzi UVCCM Arusha ni vurugu tupu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
INASEMEKANA huyu mwanadada ndiye aliyevunja rekodi ya watu weusi duniani maana maranyingi watu walisubiri atabasamu ili waamin...
-
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufund...
-
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inatoa nafasi nyingine kwa watu wenye sifa za kujiunga na vyuo vikuu kutuma maombi yao kwa msimu wa...
-
Majuto anasema kuwa ana watoto tisa ingawa hakuwa tayari kuwazungumzia mama wa watoto hao zaidi ya kumwongelea mkewe wa sasa, A...
No comments:
Post a Comment