Tuesday, September 10, 2013

MLUGO AJIPANGA KUDHIBITI UDANGANYIFU KWENYE MTIHANI WA DARASA LA SABA

Wakati leo darasa la saba wakiwa wameanza mitihani yao itakayofanyika kwa siku mbili yaani leo na kesho, Naibu Waziri wa Elimu nchini Bw Philip Mlugo ametoa namba zake za simu kupitia vyombo vya habari ili tu kama kutakuwa kuna jambo lolote litakalohusisha udanganyifu katika mtihani huo aweze kupewa taarifa.
Namba hizo za waziri wa elimu ni 0754 315 922. Hivyo watanzania wote watakaobaini udanganyifu wowote utakaojitokeza kwenye mtihani huo wa darasa la saba sehemu yoyote nchini apate kumpigia simu kupitia namba hizo nakumpatia taarifa kamili kuhusiana na tukio hilo

No comments:

Zilizosomwa zaidi