WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Hamis Kagasheki ametangaza
kuwachukulia hatua za kinidhamu maofisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya
Ngorongoro (NCAA) waliokwamisha mradi wa kuwasaidia wafugaji wa hifadhi
hiyo ulioahidiwa na Rais Jakaya Kikwete mwaka 2008.
Akizungumza na wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro na viongozi wa
NCAA mara baada ya kuelezwa kuhusu kukwama kwa mradi huo, Balozi
Kagasheki alisema lazima hatua kali zichukuliwe dhidi ya viongozi hao.
“Haiwezekani mradi ulioahidiwa mwaka 2008 leo
hii ukwame, waliohusika kuukwamisha ni lazima wakae pembeni. Ninakwenda
Dar es Salaam ila wakae wakijua kuwa barua zao zinakuja” alisema
Kagasheki na kuongeza;
“Kabla sijaondolewa wizarani kutokana na matatizo kama haya, mtaondoka
ninyi kwanza.…, kukwama kwa mradi huu kutawafanya wananchi wamchukie
Rais Kikwete na wanasiasa,” alisema Balozi Kagasheki.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
-
Kaimu Mkurugenzi wa SUMATRA Athman Kilima akizungumza na waandishi wa habari leo April 02,2013 katika makao m...
-
-
Manfred Adam anayekabiliwa na kesi ya kutishia kuua katika hali isiyotarajiwa amelimwaga kojo katika Mahakama ya Mwanzo na kuleta vurugu ...
-
MTUHUMIWA wa mauaji ya watu tisa na unyang'anyi wilayani Tarime mkoani Ma...
No comments:
Post a Comment