Wednesday, May 7, 2014

TAZAMA PICHA ZA MAHABUSU WALIOVUA NGUO NA KUBAKI UCHI KATIKA MAHAKAMA WILAYA YA NYAMAGANA JIJINI MWANZA


Askari Polisi wakiwalinda mahabusu wawili kati ya Sita wanaotuhumiwa kwa kesi za mauaji, wakiwa wameng'ang'ania mlingoti wa Bendera ya Taifa huku mnoja akiwa mtupu mara baada ya kutoroka toka kwenye msafara wa mahabusu waliokuwa wakiingia mahakama ya wilaya ya Nyamagana na kisha mmoja wao kuvua nguo-Mei 07,2014.


Inspector Henry akiwasihi mahabusu hao wawili wanaotuhumiwa kwa kesi za mauaji, kuachia mlingoti wa Bendera ya Taifa na kurudi kwenye chumba cha mahakama kwaajiri ya taratibu za kesi.


Inspector Henry (shati la bahari) akiwa na Inspector Veda (mwenye koti) wakisikiliza hoja za  Thobiasi Warioba (35), aliyeamua kuvua nguo zote na kubaki mtupu akiwa ameng'ang'ania mlingoti wa Bendera ya Taifa uliopo katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Nyamagana mkoa wa Mwanza, ambaye anakabiliwa na kesi ya mauaji Na. 32/2012.


Inspector Veda (mwenye koti) akichukuwa maelezo ya Thobiasi Warioba (35), aliyeamua kuvua nguo zote na kubaki mtupu akiwa ameng'ang'ania mlingoti wa Bendera ya Taifa uliopo katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Nyamagana mkoa wa Mwanza, ambaye anakabiliwa na kesi ya mauaji Na. 32/2012. akiwa na mwenzake Hamis Ramadani (30).


Mahabusu Thobiasi Warioba (aliye mtupu) pamoja na mwenzake Hamis Ramadhani katu katu waking'ang'ania mlingoti wa bendera ya Taifa huku wakishinikiza kuzungumza na waandishi wa Habari.


Wananchi wamefurika viwanja vya mahakama kushuhudia tukio hilo la Mei 07,2014..........


Baada ya kuzungumza na waandishi wa habari mahabusu hao walikubali kurejea chumba cha Mahakama.



Wananchi wamefurika viwanja vya mahakama kushuhudia tukio hilo la Mei 07,2014.........

No comments: