Wednesday, December 18, 2013

MAN UNITED WATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA LIGI, SPURS NJE LICHA YA ADEBAYOR KUFUNGA

KOCHA David Moyes ameendelea kupambana baada ya jana kuiongoza Manchester United kushinda mabao 2-0 dhidi ya Stoke City katika Kombe la Ligi England.
Ushindi huo wa United jana ulitokana na mabao ya Ashley Young dakika ya 61 na Patrice Evra dakika ya 78.
article-2526024-1A2FC12600000578-769_634x439_13a0d.jpg
Katika mchezo mwingine, mshambuliaji Emmanuel Adebayor alirejea uwanjani na kufunga bao moja wakati timu yake, Tottenham Hotspur ikifungwa 2-1 na West Ham United, mabao ya Jarvis dakika ya 80 na Maiga dakika ya 85.
Man United sasa itamenyana na Sunderland katika Nusu Fainali ya michuano hiyo maarufu kama Capital One, wakati West Ham itakipiga na Manchester City.
Adebayor akishangilia bao lake ambalo hata hivyo halikuweza kuinusuru Spurs na kipigo
Nayo Manchester City iliifunga 3-1 Leicester na kufikisha jumla ya mabao 75 katika mechi 25 za mashindano yote msimu huu.
article-2525815-199D593100000578-596_634x494_a8818.jpg
Free-scoring: Sergio Aguero (centre) and Alvaro Negredo (left) are combining effectively in Manchester(P.T)

No comments:

Zilizosomwa zaidi