Friday, September 13, 2013

CCM YAPOTEZA NAFASI YA MEYA MJINI MUSOMA

Diwani wa kata ya mwisenge kwa tiketi ya chama cha demokrasia na maendeleo mh. Bwire Nyamwero leo ametangazwa kuwa naibu meya wa halmashauri ya manispaa ya Musoma baada ya kumshinda diwani wa kata ya Nyasho kwa tiketi ya CCM Goldon Mumbala katika uchaguzi wa kumtafuta naibu meya wa manispaa ya Musoma. 

Mkurugenzi wa manispaa ya Musoma ahmed sawa ametangaza bwire kama mshindi na kwamba amemshinda mpinzani wake kwa kura 11 kwa 5.
Jumla ya madiwani 17 wameshiriki katika zoezi hilo ambapo kura moja imeharibika kati ya kura 16 zilizopigwa.
Akizungumza baada ya kutangazwa mshindi mh. bwire amesema amefurahi kuchaguliwa tena katika nafasi hiyo na hivyo kuupongeza kamati ya uchaguzi huku akiahidi kutoa ushirikiano kwa baraza la madiwani.
Amewaomba wananchi wamuunge mkono ili aweze kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.
naye diwani mumbala wa chama cha mapinduzi ameyakubali matokea hayo na kuahidi kushirikiana kwa moyo mmoja na naibu meya huyo ili kutekeleza shughuli mbalimbali za baraza hilo ikiwa ni pamoja na kushirikiana na baraza ili kufanikisha ipasavyo maendeleo ya halmashauri.
Baada ya uchaguzi wa naibu meya baraza hilo la madiwani liliahirisha kikao hicho kwa muda ambapo baadae kiliikaa tena kwaajili ya kufanya uchaguzi wa kamati za kudumu ambapo Mh. Haile S. Sarai. alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya mipango miji maliasili na mazingira
Hata hivyo kamati ya elimu afya na huduma za jamii haikuweza kupata kiongozi wake kwa kuwa kamati hiyo haikufanya uchaguzi
kufuatia hali hiyo kamati ya elimu afya na huduma za jamii imepanga kufanya uchaguzi ndani ya siku 30 ili kumpata mwenyekiti wake

No comments:

Zilizosomwa zaidi