MAANDAMANO ya amani yaliyokuwa
yameandaliwa na chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) yamegeuka yaligeuka
na kusababisha kuotea kwa amani ya wakazi wa jiji la Mwanza baada ya kuibuka
mapambano makali baina ya waandamanaji na jeshi la polisi mkoani Mwanza na
kusababisha polisi kutumia nguvu kuwatawanya wafuasi wa chama hicho.
Maandamano hayo ya amani ambayo
yalianzia katika eneo la Buzuruga nje kidogo ya jiji la Mwanza yalikuw
ayakiongozwa na wabunge Highness Kiwia wa Ilemela pamoja na Ezekiel Wenje
kuelekea katika viwanja vya Furahisha yalilenga kumshinikiza Mkuu wa Mkoa wa
Mwanza Ernest Ndikilo kutoa barua zinazodaiwa kuandikwa na ofisi ya Waziri Mkuu
Tamisemi kuwarejesha madiwani watatu waliotimuliwa katika Manispaa ya Ilemela
kutokana na kushindwa kuhudhuria vikao vitatu mfululizo.
Polisi wenye silaha pamoja na
askari kanzu walianza kutanda katika eneo hilo la Furahisha wakiongozwa na Mkuu
wa upelelezi wa makosa ya jinai Mkoa wa Mwanza RCO Konyo ambaye alikuwa
akitumia gari lenye namba za usajili DK 068EXV aina ya Toyota Land Cruiser
Maandamano hayo ambayo awali
yalionekana kana kwamba yangelimalizika salama yaliwasili katika viwanja vya
Furahisha majira ya saa 5.38 huku yakiongozwa na gari la polisi lenye namba za
usajili za nchi ya Uganda 779 UAG likiwa nimesheheni polisi wenye
silaha nzito ikiwa ni pamoja na mabomu ya machozi na bunduki pamoja na askari
kadhaa ambao walikuwa katikati ya maandamano hayo.
Baada ya maandamano hayo kuwasili
katika viwanja vya Furahisha kwa amani,waandamani hao ambao walikuwa na mabango
mbalimbali yaliyosomeka kuwa ‘Matata hatutaki uendelee kuwa Meya wa Ilemela
rudia kazi yako ya awali, na jingine Jaji Sumari tumechoka kuahirisha mara kw
amara kesi dhidi ya Matata na jingine lililosomeka kuwa RD Ndikilo
tunahitaji barua za kurejeshwa kwa madiwani wetu.
Hata hivyo tofauti na ilivyokuwa
imetangazwa kuwa maandamano hayo ya amani yangelipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa
Mwanza Ernest Ndikilo,hakukuwa na kiongozi yoyote wa Serikali ambaye alikuwepo
uwanjani hapo kupokea maandamano hayo.
Kufuatia kutoonekana kwa kiongozi
yoyote wa Serikali,viongozi wa chadema pamoja na wabunge wao walikutana kwa
faragha kwa dakika kadhaa kwa ajili ya kujua hatima ya maandamano hayo ambapo
Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje alipanda jukwaani saa 6.45 na kuwaeleza
maelfu ya waandamanaji kuwa wameamua kumtuma Mbunge wa Ilemela Highnes Kiwia
kwenda ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kuchukua majibu kwa ajili ya
kuwaletea wananchi walioandamana juu ya hatima ya madiwani hao.
Hata hivyo saa moja baadae Mbunge
huyo alisimama jukwani na wakuwaeleza waandamani hao kuwa simu ya Mbunge Kiwia
ilikuwa haipatikani hivyo kuwataka kuandamana kwenda kwa Mkuu wa mkoa wa Mwanza
kujua kulikoni na hapo ndipo hali ya hewa ilipochafuka.
Jeshi la polisi baada ya kuona wandamanaji
hao wameanza kuelekea katika ofisi za Mkuu wa mkoa liliwataka kutawanyika
ambapo waandamanaji hao walikaidi ndipo jeshi la polisi lilipoamua kutumia
mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi hao.
Vurugu hizo ambazo zilianza majira
ya saa 7.30 zilisababisha kufungwa kwa baadhi ya barabara kutokana na
waandamanji hao kuweka vizuizi vya mawe na kuchoma matairi,ambapo pia maduka na
ofisi mbalimbali zililazimika kufungwa kwa muda kupisha vurugu hizo.
Baadhi ya wananchi ambao walikuwa
wakitumia usafiri wa umma walionekana wakishuka kupitia katika madirisha ya
magari hayo na kukimbia kwa hofu ya kujeruhiwa na mabomu pamoja na mawe ambayo
yalikuwa yakirushwa na waandamanji hao kwa jeshi la polisi.
No comments:
Post a Comment