Pia, wanawake wamekuwa wakipenda usafi wao binafsi, wakitumia vitu ambavyo baadhi yake ni hatari.
Wapo baadhi ya wanawake wanaopenda kusafisha
sehemu zao za siri kwa kutumia sabuni zenye kemikali, marashi (pafyumu)
au kupaka mafuta.
Kwa maelezo ya wataalam, hao wapo hatarini kupata magonjwa ya zinaa au ya kuambukiza.
Watafiti katika Chuo Kikuu cha California, Marekani wanasema sabuni ngumu au hata za maji, pafyumu (deodorant) zinaharibu tishu muhimu zilizomo ndani kabisa ya uke na kumweka mhusika katika hatari ya kupata malengelenge, fangasi na hata Ukimwi.
Watafiti katika Chuo Kikuu cha California, Marekani wanasema sabuni ngumu au hata za maji, pafyumu (deodorant) zinaharibu tishu muhimu zilizomo ndani kabisa ya uke na kumweka mhusika katika hatari ya kupata malengelenge, fangasi na hata Ukimwi.
Aidha, sabuni au dawa zinazouzwa na
wafanyabiashara zikitangaza kuboresha uke au kuondoa harufu kwenye
sehemu hizo nyeti nazo zimeelezwa kuwa na madhara.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Cyriel Massawe anasema sabuni au mafuta yenye kemikali huchubua ngozi laini ya uke na ni rahisi vimelea vya magonjwa kuenea kwa urahisi.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Cyriel Massawe anasema sabuni au mafuta yenye kemikali huchubua ngozi laini ya uke na ni rahisi vimelea vya magonjwa kuenea kwa urahisi.
Dk Massawe anasema michubuko hiyo ambayo si rahisi kuonekana kwa macho ndicho chanzo cha kuingia kwa maradhi ya kuambukiza.
“Hamna haja ya kuweka kemikali, au pafyumu ukeni. Hizo sehemu zinahitaji kuoshwa vizuri kwa maji,” anasema Dk Massawe.
“Hamna haja ya kuweka kemikali, au pafyumu ukeni. Hizo sehemu zinahitaji kuoshwa vizuri kwa maji,” anasema Dk Massawe.
Anasema kemikali inapoingia ukeni inavuruga hali ya kawaida na asidi inayolinda sehemu hizo.
Anaongeza kuwa ni vyema wanawake wakaelimishwa
kuhusu matumizi ya bidhaa zinazodaiwa kuweka harufu nzuri katika
sehemu zao za siri, kurudisha bikira au mafuta ya kulainisha uke.
Naye Daktari Bingwa wa Kitengo cha Patholojia MNH,
Henry Mwakyoma anasema wanawake wanaofanya usafi sehemu zao za siri kwa
kutumia bidhaa au baadhi ya vifaa visivyofaa kutumiwa ukeni huweza
kupata saratani ya shingo ya uzazi.
Dk Mwakyoma aliyewahi kufanya utafiti kuhusu
saratani ya shingo ya kizazi nchini anasema, bidhaa zenye kemikali ya
‘coal tar,’ ambazo mara nyingine huwekwa kwenye sabuni ama manukato na
kutumiwa ukeni na wanawake huweza kuchochea saratani hiyo.
Kiongozi wa utafiti huo, Dk Joelle Brown, alisema
upo ushahidi wa kutosha kuwa kutumia sabuni za kuogea za maji au ngumu
katika sehemu za siri za ndani za mwanamke kunaharibu uwiano wa bakteria
na kusababisha bakteria kuzalishwa kwa wingi na kumweka mwanamke katika
hatari ya maradhi ya zinaa ya kuambukiza.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
No comments:
Post a Comment