Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimekubali kusitisha
maandamano yaliyokuwa yafanyike leo kushinikiza kujiuzulu Waziri wa
Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa kutokana na matokeo
mabaya ya kidato cha nne ya 2012.
Makubaliano yalifikiwa baada ya kikao cha Mkuu wa
Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Said Mwema na viongozi wa Chadema
walioongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe kilichofanyika
makao makuu ya jeshi hilo jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment