Kwa ushindi huo, Stars sasa imefikisha pointi sita
na hivyo kuendelea kushika nafasi ya pili katika Kundi C ikiwa nyuma ya
Ivory Coast yenye pointi saba, baada ya kuifunga Gambia mabao 3-0 juzi.

Stars ilianza mchezo huo kwa kasi na kulifikia
lango la wapinzani wao dakika ya pili tu ya mchezo wakati shuti la
kiungo Amri Kiemba ilipogonga mtambaa wa panya kabla ya mabeki wa
Morocco kuon-doa mpira kwenye hatari.
Dakika ya tisa Morocco ilijibu mapi-go na kona
iliyochongwa na Barrada Abdellaziz ilimfikia Abuurazouk Hamza ambaye
alipiga kichwa kilichotoka senti-mita chache kwenye lango la Stars.
Baada ya kashikashi hizo, kila upande ulijaribu
kutuliza mpira chini na kupelekeana mashambulizi kwa zamu. Hata hivyo
hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika hakuna timu ili-yokuwa
imetingisha nyavu.
No comments:
Post a Comment