Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Bw. John
Nkolo (aliyesimama) akijitambulisha kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe.
Magesa Mulongo wakati Wajumbe wa Tume hiyo walipokwenda kujitambulisha
kwake kabla ya tayari ya kuanza kazi ya ukusanyaji wa maoni ya wananchi
kuhusu Katiba Mpya katika Mkoa huo. Wajumbe wengine ni Bw. Abubakari
Ali, Bw. Ussi Ali na Bi. Mwantumu Malale.
Mkuu
wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo (wa pili kulia) akiwa katika picha ya
pamoja na wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba mara baada ya wajumbe
hao kujitambulisha kwake tayari kuanza kazi ya ukusanyaji wa maoni ya
wananchi kuhusu Katiba Mpya mkoani humo. Kutoka kushoto ni Bw. Abubakari
Ali, Bw. Ussi Ali, Bi. Mwantumu Malale (na wa kwanza kulia) Bw. John
Nkolo.
Mjumbe
wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Bi. Mwantumu Malale akizungumza wakati
wajumbe wa Tume hiyo walipokwenda kujitambulisha kwa Mkuu wa Mkoa wa
Arusha tayari kuanza kazi ya ukusanyaji wa maoni ya wananchi kuhusu
Katiba Mpya mkoani humo. Kulia ni Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Magesa Mulongo.
No comments:
Post a Comment