Sunday, November 18, 2012

POLISI KENYA, WAENDELEA KUWASAKA WEZI WA MIFUGO.

Mifugo nchini KenyaBaada ya wizi wa mifugo uliotikea juzi nchini Kenya, Polisi wa nchi  bado wanaendelea na harakati za kuwasaka wezi wa mifugo waliosababisha mauaji ya takriban polisi 42 katika eneo la Baragoi kaskazini mwa nchi hiyo.
Polisi wengine zaidi ya 20 wanapokea matibabu katika hospitali kuu ya Kenyatta nchini humo. Maafisa hao wa polisi walikuwa katika harakati za kuwatafuta n'gombe walioibiwa wakati waliposhambuliwa na wezi wa mifugo.
Tayari polisi ya Kenya imetangaza vita dhidi ya wezi wa mifugo na maafisa kadhaa wa polisi wamepelekwa katika eneo hilo kuendeleza msako 

                                                                                       mkali wa majangili hao.

No comments:

Zilizosomwa zaidi