
Utaratibu huo unasababisha kukosekana kwa uwiano katika utaoji wa elimu baina ya shule za mijini na vijijini.
Wanafunzi hao walitoa malalamikoa hayo juzi
kupitia Baraza la Watoto la Wilaya ya Kilwa, lilipokuwa
likizungumza na timu ya waandishi wa habari waliotembelea baraza hIilo
kwa ufadhili wa Shirika la Save the Children.
Akizungumza kwa niaba ya baraza la watoto la
wilaya hiyo, Idrisa Samli, alisema moja ya kero na sababu
zinazochangia kuzohofisha morali ya watoto kutopenda shule, ni pamoja
na kitendo cha watendaji na viongozi wa halmashauri hiyo, kutoa
upendeleo kwa ndungu na wake zao, kufundisha shule za mijini.
Samli alisema kitendo hicho ndiyo chanzo cha
kukithiri kwa tatizo la utoro miongoni mwa wanafunzi na tofauti katika
uatoaji wa elimu kati ya shule za mjini na vijiji .
Alielezea kushangazwa kwake kuona viongozi wa
elimu katika wilaya hiyo, hawalichukulii suala hilo kama sehemu ya
matatizo yanayochangia kushusha kiwango cha taluuma.
Baraza hilo limeuomba uongozi wa wilaya,
kuangalia uwezekano wa kuwapunguza walimu wanaofundisha mijini na
kuwapeka vijiji ambako kuna upungufu mkubwa wa walimu.
Limesema hatua hiyo itasaidia kuleta wiano wa walimu na wanafunzi katika shule za mijini na vijijini.
No comments:
Post a Comment