
Paluku amesema wanajeshi 150 wa waasi wameuawa lakini msemaji wa waasi hao amekanusha habari hizo.
Mapigano hayo ndiyo mabaya zaidi tangu mwezi Julai mwaka huu katika eneo hilo lenye utajiri mkubwa wa madini.
Zaidi ya watu laki tano wamehama makwao tangu mwezi Aprili mwaka huu, wakati wanajeshi kadhaa walipoasi kutoka kwa jeshi la Serikali.
Mapigano hayo yamekuwa yakiendelea karibu na kijiji cha Kibumba takriban kilomita 30 Kaskazini mwa Goma.
No comments:
Post a Comment