Saturday, October 13, 2012

MAKANISA YALIYOCHOMWA DAR YAFIKA SABA.


Wakati idadi ya makanisa yaliyochomwa moto  kutokana na vurugu zilizotokea juzi Mbagala Kizuiani jijini Dar es Salaam ikifikia saba, viongozi wa madhehebu mbalimbali ya Kikristo wameonya kuwa, Serikali ikishindwa kudhibiti matukio ya vurugu za kidini, taifa linaweza kuingia katika umwagaji damu.Vurugu hizo zilitokea juzi baada ya watu wanaodaiwa kuwa waumini wa dini ya Kiislamu kuvamia Kituo cha Polisi, wakitaka wapewe  mtoto aliyedaiwa kudhalilisha kitabu kitakatifu cha Quran kwa kukikojolea.

No comments:

Zilizosomwa zaidi