Tuesday, February 4, 2014

OPERESHENI TOKOMEZA UJANGILI AAMU YA PILI KUANZA


tanzania-poaching-elephants-340 2271 51908


WIZARA ya Maliasili na Utalii, imesema inakabiliwa na upungufu wa askari 3767 wa wanyamapori wanaohitajika katika kupambana na matukio ya ujangili. (HM)
"Kampeni ya Tokemeza Ujangili, itaanza kwa awamu ya pili na tumejipanga kuhakikisha hakuna kasoro zitakazojitokeza. Tunahitaji askari 4855, lakini mpaka sasa tunao askari 1088 ambao hawatoshelezi kuendesha kampeni hiyo," alisema Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyarandu.
Nyalandu pia amesema askari wote waliohusika katika hatua ya kwanza ya kampeni ya Tokomeza Ujangili ambayo ilisimamishwa kutokana na kasoro zilizojitokeza huku wakiwa hawajapewa haki zao, wanatambulika.
Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana katika mkutano wa majadiliano na wadau mbalimbali wa maendeleo uliolenga kutafuta mbinu thabiti ya kupambana na ujangili.
Nyalandu alisema askari wote watapatiwa haki zao kwa sababu Serikali inawatambua .
"Tunaamini tutapata askari wa kutosha kwa sababu katika ili hatuko peke yetu bali tunashirikiana na wenzetu kutoka katika vyombo vya usalama wakiwamo polisi na Jeshi la Wananchi," alisema.
Alisema Benki ya Dunia imesema ipo tayari kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Tanzania katika kampeni hiyo ya awamu ya pili.
"Nichukue nafasi hii kuwashukuru Benki ya Dunia kwa kukubali na kuitikia wito uliotolewa na Rais Kikwete alipowataka wadau wa maendeleo kujitokeza kutusaidia katika kampeni hizi na wao wameonyesha utayari wao leo," alisema Nyalandu. 

No comments: