Tuesday, February 4, 2014

MATATA: NIMECHOSHWA NA SIASA ZA KINAFIKI

11 81d79
MEYA wa Manispaa ya Ilemela kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Henry Matata amesema anatarajia kurejea katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwakani
Amesema atachukua hatua hiyo baada ya kuchoshwa na siasa za unafiki, ubabe, majungu na ukabila ndani ya Chadema.
Akizungumza nyumbani kwake, Matata alisema anajuta kujiunga na Chadema na kutumia gharama zake kubwa kukiimarisha na kujikuta akifukuzwa kutokana na majungu.
Matata amewapiga vijembe viongozi wakuu wa Chadema kuwa wamepoteza uelekeo na wanakiua chama hicho kutokana na kutokubali ushauri wa kukinusuru chama hicho.
Alisema ameamua kurejea CCM mwaka 2015 kutokana na mazingira yalivyo ndani ya Chadema kwa sasa ambako hakuna matumaini tena kutokana na mgogoro wa kung'ang;ania madaraka hali ambayo imekidhohofisha chama hicho.
Matata alisema kabla ya kukimbilia Chadema alikuwa ndani ya CCM lakini kutokana na kutokutendewa haki aliamua kukimbia kwa kudhani kile anachokipigania atakwenda kukipata ndani ya chama hicho lakini hali aliyoikuta kule ni tofauti.
Alisema kwake CCM ni kama nyumbani ndiyo maana hajuti kurejea mwakani na kuwania nafasi yoyote kutokana na mazingira yatakavyokuwa kwa wakati huo.
Matata alitamba kuwa anatarajia kuleta mtikisiko mkubwa ndani ya Chadema mwaka atakapoondoka na idadi kubwa ya wanachama wakiwamo madiwani ambao wamekuwa wakimuunga mkono. Chanzo: mtanzania

No comments: