Monday, February 10, 2014

KIJANA AKUTWA AMEJINYONGA KISA UGMU WA MAISHA

nyongaKijana huyu aliyetambulika kwa jina moja la Bahati ambaye alikuwa akijishughulisha na uuzaji wa mifuko ya plastiki maarufu kama rambo amekutwa akiwa amekufa baada ya kujinyonga juu ya mti jirani na ufukwe huko mjini Bukoba mkoani Kagera.

Ufukwe huo ambao upo jirani kabisa na stand ya mabasi ya mkoani humo na marehemu alionekana akifua nguo zake na ndipo baadae kisa kikawa mkasa kijana huyu akafikwa na haya yaliyomfika.
Mwili wa marehemu umepelekwa hospitali kwa kuhifadhiwa kwa ajili ya utambuzi na utaratibu mwingine kuendelea.

Waandishi na mashuhuda wakishuhudia tukio
Mwili wa marehemu ukiwa umeshushwa tayali kwa safari ya hospitali

No comments:

Zilizosomwa zaidi