Friday, September 13, 2013

MOTO WATEKETEZA NYUMBA MBWENI,WATOTO NA WAZAZI WANUSURIKA

Ni kuamkia leo asubuhi ya Tar.14/09/2013 huko mbweni pembezoni mwa jiji la Dsm,nyumba moja ya Ofisa mmoja wa UN Mtanzania huko SUDAN imeteketea kabisa kabisa kwa moto usiku wa Manane.Inasemekana moto umeanzia kwenye chumba cha watoto na haijafahamika kama ni hitirafu ya umeme au la?
Bahati mbaya sana hakuna kitu kilichookolewa hata kimoja,mali zote zimeteketea kwa moto na hakukuwepo na jitihada zozote za kuuzima kutokana na muda wa moto ulipoanza pia majirani hawakuwa na uwezo wa kudhibiti moto huo kwa sababu ulishika eneo kubwa la nyumba hiyo.

No comments:

Zilizosomwa zaidi