Mmoja wao aliangua kilio na kuanguka baada ya kutangazwa kwa hukumu dhidi yao .
Msichana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 23 aliumizwa sana na baada ya wiki moja alifariki kutokana na majeraha .
Karibu miezi 9 baada ya ubakaji ulioitikisa
India, jaji ametoa hukumu kwa wanaume wote wanne ambao tayari walikuwa
wamepatikana na hatia ya uhalifu .
Wendesha mashtaka walikuwa wamewaombea hukumu ya
kifo wakisema ingetoa ishara muhimu kwamba uhalifu wa aina hiyo
hautakubalika kamwe .
Familia ya mwanamke huyo pia waliomba wanaume hao wanyongwe .
Lakini mawakili watetezi wa wanaume hao
walipinga mapendekezo ya hukumu ya kifo , wakisema wateja wao hawakuwa
na rekodi za uhalifu awali na kwamba wanastahili kusamehewa .
Kifo cha mwanafunzi huyo mwezi Disemba mwaka
jana kilisababisha maandamano makubwa ya upinzani kote nchini India ,
yaliyoilazimisha serikali kubadili sheria zilizokuwepo za uhalifu wa
ngono
BBC
No comments:
Post a Comment