Thursday, May 23, 2013

WANANCHI WATAKIWA KUPEWA ELIMU JUU YA UGONJWA WA FISTULA

 
(Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi)
Wakati leo ni Siku ya Fistula duniani huku hafla ya kitaifa ikifanyika jijini Dar es Salaam Makao Makuu ya CCBRT, wakazi wa Morogoro wametaka kampeni ya fistula kusambazwa vijijini ili kutoa somo kwa wanawake wengi wenye matatizo hayo.
Fistula ni ugonjwa unawapata wanawake wengi kwa kutokwa na haja zote kwa wakati mmoja bila kujitambua. Kampeni ya kuelimisha umma kuhusu fistula ilyoanzia mkoani Kagera imeingia mkoani Morogoro ikiwa ni kampeni ya kuelimisha umma kuhusu fistula.
Wamesema ingawa walikuwa wakifahamu kuhusu tatizo la fistula, lakini elimu hiyo iliyohusisha ushuhuda kutoka kwa baadhi ya wanawake waliowahi kukumbwa na fistula na baadaye kupata matibabu imewapa uelewa na ufahamu mpana zaidi ambao ipo haja ya kuhakikisha ujumbe huo unafika kila kona ya nchi hususan vijini.
“Nimefurahi sana nimeelimika vya kutosha kuhusu fistula. Mwanzoni nilifika hapa kumshuhudia Msanii Mwana FA lakini mawazo yangu yalibadilika ghafla na kujikuta naguswa na elimu ya fistula.”alisema Emmanuel Nyangaka.
Kwa upande wake pamoja na kupongeza juhudi za Vodacom pamoja na kuuliza maswali kadhaa, mkazi mwingine Hassan Ndungate alisema elimu hiyo ni fusra ya kipekee kwa jamii kujua mambo mbalimbali yanayohusu fistula ili waweze kutoa msaada au na kuhamamisha jamii kujitokeza kupata matibabu.
Alishauri elimu hiyo iendelee hadi vijiji mbalimbali.     


No comments:

Zilizosomwa zaidi