Sunday, March 24, 2013

TAIFA STARS YAENDELEA KUFANYA VIZURI KATIKA KUFUZU KUCHEZA KOMBE LA DUNIA 2014.

Mabao matatu ya nyota wa TP Mazembe ya DR Congo, Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu yalitosha kuipa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ ushindi mnono wa mabao 3-1 dhidi ya Morocco katika mechi ya kutafuta tik-eti ya kufuzu kushiriki Fainali za Kombe la Dunia, Brazil 2014.

Kwa ushindi huo, Stars sasa imefikisha pointi sita na hivyo kuendelea kushika nafasi ya pili katika Kundi C ikiwa nyuma ya Ivory Coast yenye pointi saba, baada ya kuifunga Gambia mabao 3-0 juzi.
Mshambuliaji Ulimwengu aliyeingia akitokea benchi kipindi cha pili alifunga bao la kwanza la Stars dakika ya 46, kabla ya kumtengenezea nyota mwenzake wa TP Mazembe, Samata aliyefunga mengine mawili dakika ya 66 na 80.

Stars ilianza mchezo huo kwa kasi na kulifikia lango la wapinzani wao dakika ya pili tu ya mchezo wakati shuti la kiungo Amri Kiemba ilipogonga mtambaa wa panya kabla ya mabeki wa Morocco kuon-doa mpira kwenye hatari.

Dakika ya tisa Morocco ilijibu mapi-go na kona iliyochongwa na Barrada Abdellaziz ilimfikia Abuurazouk Hamza ambaye alipiga kichwa kilichotoka senti-mita chache kwenye lango la Stars.

Baada ya kashikashi hizo, kila upande ulijaribu kutuliza mpira chini na kupelekeana mashambulizi kwa zamu. Hata hivyo hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika hakuna timu ili-yokuwa imetingisha nyavu.

No comments:

Zilizosomwa zaidi