Monday, March 18, 2013

SIKU YA KUCHAGUA MABARAZA HADI APRIL 5

Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeongeza siku mbili za kupiga kura ya kuchagua wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya, zoezi ambalo awali lilipangwa mara ya kwanza kufanyika kati ya Machi 30 mpaka Aprili 3, mwaka huu.
Mabadiliko hayo ya ratiba yamekuja baada ya baadhi ya makanisa kutumia ibada ya juzi Jumapili pamoja na mambo mengine kuonya juu ya ratiba hiyo ya Tume kuwanyima haki wafuasi wa dini ya Kikristo kutokana na siku zilizokuwa zimepangwa kuangukia kwenye Sikukuu ya Pasaka.

Katibu wa Tume hiyo, Assaa Ahmad Rashid aliieleza Mwananchi jana kuwa muda umesogezwa mpaka Aprili 5 mwaka huu badala ya Aprili 3 kama ilivyokuwa imetangazwa awali.

“Kwa mujibu wa mabadiliko mapya, vikao hivyo sasa vitafanyika kati ya Machi 30 hadi Aprili 5, kwa msingi huu kila kijiji au mtaa kitachagua tarehe ambayo wananchi watapiga kura kuwachagua wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya,” alisema.

No comments:

Zilizosomwa zaidi