![Rais wa Malawi awafuta kazi wakuu wa jeshi](http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/94051cf55d661101a1e5561c95f2bcc6_L.jpg)
Odillo na Msonthi ambao wote pia waliwahi kuwa wanadiplomasia,
wanahusishwa na mgogoro wa kikatiba ulioibuka Aprili 2012 baada ya kifo
cha ghafla cha Rais Bingu wa Mutharika. Wakati Bingu alipoaga dunia
ilitazamiwa kaka yake, Peter, ambaye wakati huo alikuwa waziri wa mambo
ya nje, angechukua kiti cha urais badala ya Joyce Banda ambaye kikatiba
alitakiwa achukue nafasi hiyo lakini alikuwa amejiondoa kwenye chama
tawala. Katika harakati hizo Joyce Banda alikutana na Odillo ambaye
alimpa ulinzi kamili na kutangaza kuunga mkono urais wake. Kufuatia
uungaji mkono wa jeshi, Banda alitawala hadi Mei mwaka huu wakati
uchaguzi wa rais ulipofanyika na Peter Mutharika kuibuka mshindi licha
ya kuwepo madai ya wizi wa kura.
Jeshi la Malawi pia limehusishwa na kashfa ya ufisadi ambayo imepewa
jina la 'Cashgate' ambapo mamilioni ya dola ya fedha za umma yalipotea
mwaka jana.
Chanzo:Swahili Radio Tehran
No comments:
Post a Comment