Shirika la Mpango wa Chakula Duniani WFP limetangaza kuwa 
Zimbabwe licha ya kukabiliwa na upungufu mkubwa wa bajeti, 
inakabiliwa pia na upungufu mkubwa wa chakula na kutishia maisha ya 
mamia ya maelfu ya wananchi wa nchi hiyo.
Taarifa iliyotolewa na WFP 
imeeleza kuwa, shirika hilo la kimataifa linahitaji dola milioni 90 ili
 liweze kuendelea kutoa misaada ya chakula kwa taifa la Zimbabwe katika 
kipindi cha miezi sita ijayo. 
Imeeleza kuwa, shirika hilo
 linahitajia dola milioni 180 ili liweze kutoa misaada yake kikamilifu 
kwa nchi za Kusini mwa Afrika kama vile  Zimbabwe, Msumbiji, Madagascar 
na Jamuri ya Kidemokrasia ya Kongo. 
Naye  Mkuu wa Kitengo cha 
Mawasiliano cha WFP mjini Johannesburg nchini Afrika KusiniDavid Orr, amesema kuwa
 nchi za ukanda wa Pwani ikiwemo Madagascar zitakabiliwa na baa kubwa la
 njaa kabla ya kuanza msimu wa mavuno. 
Amesema kuwa, WFP ilishindwa 
kutoa misaada kwa wakimbizi wa Kivu Kaskazini nchini Kongo kutokana na 
matatizo ya kifedha yanayoikabili taasisi hiyo ya kimataifa.
		  	
No comments:
Post a Comment