Saturday, January 11, 2014

RWANDA YAKANUSHA VIKALI KIFO CHA RAIS PAUL KAGAME

Ofisi ya Rais wa Rwanda imekanusha vikali uvumi ulioenea nchini humo na nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwamba Rais Paul Kagame wa nchi hiyo amefariki dunia. 
Taarifa zinasema kuwa, uvumi wa habari za kufariki dunia Rais Kagame, zimeamsha furaha hasa kwa wakaazi wa miji ya mpaka wa nchi hiyo na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. 
Mara kadhaa Rwanda imekuwa ikituhumiwa kwa uingiliaji wa kijeshi katika maeneo ya mpaka na Kongo. Hivi karibuni Umoja wa Mataifa ulitoa taarifa na kuituhumu tena serikali ya Kigali kwa kuyaunga mkono makundi yanayobeba silaha na hasa waasi wa zamani wa M23 waliokuwa mashariki mwa Kongo. 
Hata hivyo ripoti hiyo ya Umoja wa Mataifa imekosolewa vikali na serikali ya Rwanda. Rais Paul Kagame mwenye umri wa miaka 56 aliiingia madarakani mwaka 1994, baada ya kutokea mauaji ya kimbari yaliyopelekea watu wasiopungua laki nane hasa wa kabila la Kitutsi kuuawa nchini humo.

No comments:

Zilizosomwa zaidi