Baadhi
 ya wanafunzi wa shule ya Msingi Muungano na Mpanda katika wilaya yam 
panda wakiwa nje ya Madarasa muda mfupi mara baada ya kumaliza mtihani 
wa somo la sayansi lililoanza asubuhi   kama walivyokutwa na mpiga 
 
Baadhi
 ya wananchi wa kijiji cha Tukoma wakiwa na Afisa Elimu Mkoa wa Katavi 
wakijadili mstakabali wa ujenzi wa madarasa ili kuondoa changamoto ya 
ukosefu wa vyumba vya madarasa na Nyumba za walimu shule hiyo 
inakabiliwa na uhaba wa nyumba za mwalimu na vyumba madarasa hali 
inayofanya darasa moja kusomea wanafunzi 246 wa shule hiyo ya Tukoma 
wakisoma kwa zamu, shule inawatoto kuanzia darasa la kwanza hadi la saba
 na mwaka huu watoto saba yu ndio waliofanikiwa kufanya mtihani wa 
darasa la saba. 
Wanafunzi
 wa darasa la Saba wakiwa Darasani wakifanya mtihani wa kumaliza elimu 
ya Msingi wanafunzi hao ni wa shule ya msingi Tukoma Wilaya ya Mlele .
(Picha zote na Kibada Kibada)
………………….
Kibada Kibada-Mpanda KATAVI
Afisa
 Elimu wa Mkoa wa Katavi Ernest Hinju amefanya ziara ya kushitukiza kwa 
baadhi ya shule za msingi katika wilaya ya Mpanda na Mlele na 
kuridhishwa na hali ya mtihani inavyoendelea baada ya kukuta   hali ya 
mtihani inaendelea vizuri na hakuna matatizo yeyote.
Afisa
 Elimu huyo alianza kwa kutembelea shule ya Msingi Tukoma ambayo imekuwa
 na changamoto nyingi  ikiwemo kuwa na chumba kimoja cha madarasa hivyo 
kufanya wanafunzi kuka chumba kimoja wakati wa kujifunza na kuleta 
changamot nyingi na kugonga vyomba vya habari  hivyo kufanya uongozi 
kuchukua hatua za makusudi kuhakikisha changamoto hiyo inapatiwa 
ufumbuzi.
 
 Katika ziara yake hiyo fupi alifuatana na Mkaguzi wa shule za Msingi 
 na Mjumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa na Afisa Habari   ili 
kujionea hali inavyoendelea katika maeneo mbalimbali ya shule za msingi 
ambazo wanafunzi wanaendelea kufanya Mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba 
kumaliza elimu ya Msingi.
Kwa
 upande wa Mkoa wa Katavi hali inaendelea vizuri na hakuna taarifa 
zozote zimeripotiwa za kutokea kwa matukio mabaya hali inaendelea 
vizuri.
 Afisa
 elimu Mkoa wa Katavi Ernest Hinju akiwaongea na mwandishi wa Habari 
hizi muda mfupi baada ya kutembelea shule mbalimbali za msingi 
zinazoendelea kufanya mtihani na kukuta hali iko shwari bila matatizo 
yeyote.
Baadhi
 ya shule zilizotembelewa kwa mkoa wa Katavi ni Shule ya Msingi Itenka 
B’Shule ya Msingi Dirifu na SHULE YA Msingi Tukoma ambazo zote ziko 
katika wilaya ya Mlele.
Shule
 nyingine zilizotembelewa ni shule ya Msingi 
Kashato,Katavi,Azimio,Mpanda Muungano,Majengo na shule ya Msingi Nsimbo 
ambazo ziko katika Wilaya ya Mpanda na zote hali ilikuwa shwari.
No comments:
Post a Comment