
Helikopta zenye silaha za Umoja
wa Mataifa zimeshambulia maeneo ya wapiganaji mashariki mwa Jamhuri ya
Demokrasi ya Congo, huku mapambano yanaendelea baina ya jeshi la Congo
na kundi la wapiganaji wa M23.
Kikosi cha Umoja wa Mataifa cha
kuweka amani, Monusco, kimesema kuwa vikosi vya jeshi la serikali
kaskazini ya mji wa Goma, vilishambuliwa Jumamosi asubuhi, na kufanya
raia kulikimbia eneo hilo na helikopta za Umoja wa Mataifa kutumwa huko.
Monusco ina idhini ya kuwalinda raia na kuwasaidia wanajeshi wa serikali ikihitajika.
Hakuna idadi iliyotolewa ya maafa yaliyotokea.
Umoja wa Mataifa unazilaumu Rwanda na Uganda kwamba zinawaunga mkono wapiganaji - tuhuma ambazo nchi hizo inakanusha.
No comments:
Post a Comment