Monday, October 8, 2012

Mvua kubwa zatarijia kunyesha leo.

MAMLAKA ya Hali ya Hewa nchini (TMA), imesema mvua kubwa zilizotangazwa awali zinatarajiwa kuanza leo katika mikoa ya ukanda wa pwani.Mamlaka hiyo imetangaza hali ya hatari katika ukanda huo na kuwataka wananchi kuondoka katika maeneo hatarishi ya mabondeni ambako maji hukutana.

Hivyo wakazi wa Dar es Salaam na kwingineko wamekuwa na hofu na mvua hizo kwa kuzihofia kutokana na kutangazwa mara kwa mara

Baadhi ya wakazi wa maeneo hayo tayari wameshamisha familia zao ili kukabilina na tatizo hilo

Hata hivyo hadi kufikia majira ya alasiri ya leo mvua hizo kwa mkoa wa Dar es salaam zilikuwa bado hazijaanza rasmi

Kwa taarifa iliyoipata nifahamishe zimebaini kuwa, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadik ameshajipanga kwa kuweka mikakati kwa kukabiliana na hatari hiyo.

No comments: