Saturday, August 25, 2012

Ile tabia ya abiria kujisaidi wakati wa safari maarufu kama kuchimba dawa, imekuwa ikisababisha uchafuzi wa mazingira hali ambayo sasa inapigwa vita na Serikali. Kufikia octoba mwaka huu hakuna gari litakalokuwa linasimama porini ili abiria wake wachimbe dawa. Hivyo abilia katika barabara ya Dar, Morogoro, Dodoma, Singida hadi Mwanza, wameiomba serikali kuchukua jukumu la kujenga vyoo barabarani. Wameshauri ni bora vyoo hivyo vikajengwa kila baada ya kilometa 150.

No comments:

Zilizosomwa zaidi