Thursday, August 14, 2014

MSIKITI WA KINONDONI WAUNGUA

Gari la zimamoto la Ultimate Security lililofika eneo la tukio.GPL (P.T)
Moto ukiteketeza sehemu ya chumba kimoja wapo cha jengo hilo
Raia wema pamoja na askari wakisaidiana kuuzima moto kwa kutumia mipira maalumu
Jeshi la polisi likiwa eneo la tukio kuhakikisha usalama
Msikiti maarufu wa Mtambani uliyopo Kinondoni jijini Dar es salaam waungua. Hadi muda wa saa moja na nusu usiku huu, magari ya zima moto yameonekana eneo la tukio yakijaribu kuuzima moto huo, ingawa kazi ya kuuzima imeonekana kuwa ngumu kutokana na moto kuanzia ghorofa ya juu ya msikiti huo. Magari ya zima moto yanaendelea kutafuta mbinu ya kufikisha mipira ya maji juu ya jengo hilo, ambalo chini huwa ni msikiti na juu ni madrasa. Hizi ni baadhi ya picha za tukio kama zilivyotumwa na mwandishi wa Global Publishers aliyeko eneo la tukio.
PICHA: GABRIEL NG'OSHA NA SHAKOOR JONGO/GPL

No comments:

Zilizosomwa zaidi