Wednesday, September 11, 2013

WENGER APATA PIGO

Arsenal Wenger amezidi kuchanganyikiwa na tatizo la majeruhi katika safu yake ya ushambuliaji baada ya kuumia kwa kinda lake Yaya Sanogo na kuiacha klabu ya Arsenal ikiwa na mshambuliaji mmoja pekee wa kati,Olivier Giroud .
Sanogo mwenye umri wa miaka 21 ambaye mshambuliaji  chaguo la pili  katika klabu ya Arsenal ameumia akiwa katika majukutu ya kuitumikia timu yake ya Taifa ya Ufaransa.
Nyota huyo anatarajia kupata matibabu ya nguvu makao makuu ya klabu yake, Colney HQ, Jijini London ili kumuweka sawa kabla ya klabu hiyo kusafiri kuwafuata Sunderland wikiendi hii, Huku Mesut Ozil akitarajiwa kuanza kazi rasmi siku hiyo baada ya kusajiliwa kwa ada iliyovunja rekodi ya Arsenal ya pauni milioni 42.
Blow: Yaya Sanogo injured himself on international duty with the France Under 21'sJanga: Yaya Sanogo ameumia akiwa na kikosi cha timu ya Taifa ya Ufaransa chini ya umri wa miaka 21

Pressure: Olivier Giroud is now the only fit, recognised striker at the clubPresha kubwa: Olivier Giroud ndio mshambuliaji pekee aliyefiti kwa sasa Arsenal 
Majeruhi hayo yanamaanisha Olivier Giroud amebaki mshambuliaji pekee wa kati kuelekea mchezo wa jumamosi dhidi ya Sunderland katika dimba la Stadium of Light.
Sanogo, aliyesajiliwa majira ya kiangazi mwaka huu akitokeo klabu ya Auxerre , alikuwa anatazamwa na Wenger kama mshambulaiji wa baadaye, lakini kukumbwa na uhaba wa washambuliaji alilazimika kumuweka kikosi cha kwanza.
Kushindwa kuwasajili Luis Suarez, Gonzalo Higuain, Wayne Rooney, Karim Benzema na Demba Ba majira ya kiangazi, kumemuacha Wenger na uhaba mkubwa wa chaguo la washambuliaji.
Lukas Podolski angemsaidia Giroud, lakini naye yuko nje kwa miezi mitatu kutokana na majeruhi ya nyama za oaja, wakati huo Nicklas Bendtner – anaonekana kutokuwa fiti kabisa.
Chance: Sanogo barely had a chance to impress Arsene Wenger before the injuryNafasi: Sanogo alipata nafasi adimu ya kumshawishi Arsene Wenger kabla ya majeruhi

Record breaker: Mesut Ozil was Arsenal's only major signing this summerAliyevunja Rekodi: Mesut Ozil ni mchezaji pekee aliyesajiliwa na kwa dau kubwa zaidi katika klabu ya Asernal majira ya kiangazi

No comments:

Zilizosomwa zaidi