Hanspope, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kundi la Friends of Simba, tayari ameanza vikao na wajumbe wa kundi hilo na vitaendelea leo Jumamosi. Akizungumza na Mwanaspoti, Hanspope ambaye alirejea katika nafasi hiyo katikati ya wiki hii baada ya kumaliza tofauti zake na uongozi wa Simba, alisema wikiendi hii atakuwa na vikao mfululizo na wadau wengine ili kuweka mikakati ya kuijenga klabu hiyo ya Msimbazi. Kutokana na amani iliyopo sasa, naamini mambo yatakwenda vizuri na tutapata ushindi katika mambo yetu. Waliojitoa wengi wamerudi na wengine watarudi, alisema Hanspope. Ingawa, Hanspope hakuweka wazi, Mwanaspoti linajua kuwa atakuwa na mkutano na wanachama wa Kundi la Friends of Simba ili kupanga mikakati ya mechi dhidi ya Yanga, Mei 18 mwaka huu. Ajenda nyingine zitakuwa ni kupanga mikakati ya usajili na kujadili mahali pa kuiweka kambi timu yao kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara. Hanspope, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji alisema ili Simba ipate maendeleo jambo la muhimu ni kuwa na amani. Zawadi ya amani ni ushindi, zawadi ya migogoro ni kufanya vibaya kama tulivyoona sasa, alisisitiza kapteni huyo mstaafu wa jeshi. Akiuzungumzia usajili wa msimu ujao, alisema watakuwa makini sana katika hilo, kwani msimu uliopita walifanya usajili wa pupa na wa bei mbaya ambao haujawasaidia. Tulisajili wachezaji wa bei ya juu lakini hawakutusaidia, mathalani wachezaji wa nje waliotusaidia ni kipa Abel Dhaira na Emmanuel Okwi, ambaye tayari tumemuuza, alisema Hanspope. Hanspope na baadhi ya wanachama wa Kundi la Friends of Simba walijitoa na wengine kususa kuisaidia timu hiyo kwa kilichodaiwa kuwa ni kutokubaliana na uongozi. |
Monday, April 29, 2013
SIMBA YAJIPANGA UPYA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, imeendelea leo katika viwanja tofauti na mabingwa watetezi, Yanga SC wamelazimishwa sare ya 1-1 n...
-
Ofisi ya Rais wa Rwanda imekanusha vikali uvumi ulioenea nchini humo na nchi ...
-
Dar es Salaam.Wakati nauli mpya zikianza kutumika leo huku Serikali ikizibariki, Mamlaka ya Udhibiti wa Usaf...
-
INASEMEKANA huyu mwanadada ndiye aliyevunja rekodi ya watu weusi duniani maana maranyingi watu walisubiri atabasamu ili waamin...
-
Matokeo ya Uchaguzi Mdogo jimbo la Chalinze yametangazwa Chama cha Mapinduzi CCM kimepata jumla ya kura 20812,na Chama c...
No comments:
Post a Comment