Tuesday, October 23, 2012

YANGA KUKIPIGA NA POLISI MOROGORO KESHO UWANJA WA TAIFA.


 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Kocha mkuu wa timu ya Young Africans Sports Club, Mholanzi Ernie Brandts amesema kikosi chake kipo tayari kuikabili timu ya Polisi Morogoro katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom utakaofanyika kesho uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Akiongea katika mtandao wa klabuhiyo leo asubuhi katika mazoezi yaliyofanyika shule ya sekondari Loyola, amesema wachezaji wake wote wapo safi, wana ari ya mchezo na ushindi, hivyo anaamini mchezaji yoyote atakayempanga atafanya vizuri.

Polisi Morogoro timu iliyoipanda ligi msimu huu 2012/2013 inakamata mkia katika msimamo wa ligi kuu ya Vodacom ikiwa na pointi 2 ilizozipata kwa kutoka sare michezo miwili kati ya michezo saba iliyokwishacheza.
 
Yanga ambayo mchezo wake wa mwisho iliibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya timu ya Ruvu Shooting katika mchezo uliochezwa mwishoni mwa wiki, itaingia uwanjani kusaka pointi 3 muhimu zitakazo isogeza mpaka nafasi tatu za juu na kupunguza tofauti ya point na mtani wake wa jadi Simba anayeongoza ligi kwa pointi 19.
 
Katika mazoezi yaliyofanyika leo asubuhi, kocha Brandts ameendelea kufurahia kuwepo kwa wachezaji wake wote, kitu kitakachopelea kumtumia mchezaji yoyote atakayetaka kumtumia kwa mchezo huo wa kesho, kwani hakuna mchezaji aliye majeruhi .
 
Vijana wa jangwani kwa sasa wanakamata nafasi ya tatu katika msimao wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara kwa kufikisha point 14 nyuma ya Azam yenye pointi 17 na Simba yenye pointi 19 ikiwa mbele kwa mchezo mmoja. 

Mchezo utaanza majira ya saa 10:30 jioni kwa saa za Afrika Mashariki na viingilio vya mchezo huo ni:
 
VIP A 20,000/=
VIP B &C 15,000/=
Orange 8,000/=
Blue & Green 5,000/=

No comments:

Zilizosomwa zaidi