Thursday, October 18, 2012

KANISA LA KKT LATOA TAMKO.

KANISA la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, limedai kushangazwa kwake na ukimya wa serikali pamoja na vyombo vya dola kwa kutochukua hatua mapema za vitendo vya uvunjifu wa amani vilivyokuwa vikitendeka.
Kanisa hilo pia limeeleza kusikitishwa kwake kwa vitendo vya uchomaji wa makanisa wakieleza kuwa kilichotokea Mbagala katika wiki ya kuadhimisha kifo cha Baba wa Taifa ni kebehi kwa watu waliokalia kiti chake.
Akizungumza katika ibada maalumu na kutoa salaamu za maaskofu wa kanisa hilo nchini kote kuhusiana na matukio ya kuchoma moto makanisa ya Kikristo, iliyofanyika katika kanisa la jimbo kuu Kusini Mbagala, Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini, Dk. Martin Shao, alisema kuwa wamekutana kwa madhumuni ya kuonyesha majonzi yao kwa vitendo vya uvunjifu wa amani walivyoviita ni kuporomoka kwa umoja na mshikamano wa Watanzania.
Shao pia alisema kuwa madhumuni mengine ni kupokea matumaini ya Tanzania mpya katika msiba wa wenye dini na wasio na dini.

No comments:

Zilizosomwa zaidi