Friday, September 21, 2012

Mamlaka ya dawa Tanzania yabaini dawa bandia za ARVs

MAELFU ya watu walioathirika kwa ugonjwa wa Ukimwi ambao kwa sasa wanaotumia Dawa za Kurefusha Maisha (ARVs) nchini wapo hatarini kufupisha maisha yao baada ya kubainika kuwa toleo mojawapo la dawa hizo la Machi, 2011 ni bandia.

Uchunguzi wa Mwananchi unaonyesha kuwa dawa hizo zilizosambaa katika Mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Mara zilianza kusambazwa tangu Mei mwaka huu na hadi sasa bado zipo sokoni, jambo lililoilazimu Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) kuagiza zirudishwe Bohari Kuu ya Dawa (MSD).

No comments:

Zilizosomwa zaidi