Tuesday, September 18, 2012
Askari polisi acheni wizi wakimachomacho. Inasikitisha sana kumkuta askari polisi wa kitengo cha upelelezi kufanya kazi ya askari wa usalama barabarani. Eti unamkuta askari asiyekuwa trafic kuwasumbua waendesha pikipiki (bodaboda) wakati kazi hiyo inatakiwa kufanywa na trafic. Imenisikitisha sana nilipowakuta askari wanne wakiwa umbali wa kilometa 39 kutoka mjini Kasulu mkoani Kigoma wakiwa kwenye barabara ya kuelekea kijiji cha Shunga na Buhoro, wamemsimamisha dereva pikipiki huku wakijifanya kumkagua, kama huo sio ujambazi ninini? Hivi aliyewapa wadhifa huo wa kukamata pikipiki ni nani? Na kama ni hivyo basi wakamate na magari pia sio kuwaonea bodaboda. Hawa polisi badara ya kulinda usalama wetu na mali zetu wamekuwa ni Kero sasa, jambo ambalo linawafanya baadhi ya watu wakiwaona tu, wanaanza kuogopa. Kinachoshangaza ni pale tu wanapokusimamisha, ni lazima uwaachie kiwango flani cha pesa jambo ambalo mi nathubutu kuwaita wao wezi. Polisi jaribuni kubadilika na kila mtu ahusike vizuri katika kitengo alichopo na sio ubabaishaji.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
-
Kaimu Mkurugenzi wa SUMATRA Athman Kilima akizungumza na waandishi wa habari leo April 02,2013 katika makao m...
-
-
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiongoza kikao cha NEC, leo Agosti 26, 2013 mjini Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, ...
-
Manfred Adam anayekabiliwa na kesi ya kutishia kuua katika hali isiyotarajiwa amelimwaga kojo katika Mahakama ya Mwanzo na kuleta vurugu ...
No comments:
Post a Comment