Friday, August 15, 2014

KATIBA NI NJIA KUU, WAPINGAJI NI MCHEKO

katibu wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mufindi Miraji Mtaturu,akizungumza na wananchi wa Ndolezi wakati wa ziara yake Wilayani Mufindi
katibu Muenezi wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mufindi Daud Yasini,akizungumza na wananchi wa kinyanambo Wilayani Mufindi
katibu wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mufindi Miraji Mtaturu,akimkabidhi bendera Balozi wa shina namba 15, wakati wa ziara yake Wilayani Mufindi
katibu wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mufindi Miraji Mtaturu, akiwasalimu wanachama wa CCM shina namba 15, wakati wa ziara yake Wilayani Mufindi
katibu wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mufindi Miraji Mtaturu,akizungumza na wananchi wa kinyanambo wakati wa ziara yake Wilayani Mufindi
Bila Damu katika mwili wa binadamu ni vigumu sana kuitwa Binadamu kwani ni kiungo pacha katika maisha ya binadamu, Binadamu anapitia hatua kuu tatu awapo duniani ikiwa ni pamoja na hatua ya kwanza ya kuzaliwa, ya pili ni kuoa/kuolewa na mwisho ni kifo.
Katika hatua hizo zote kuna wakati atahitaji kupata elimu juu ya ujairiamali ama elimu yeyote inayoweza kumkomboa kutoka katika utumwa wa fikra finyu.

Nilimnukuu katibu wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mufindi Miraji Mtaturu, alipokuwa akizungunza na wananchi wa Kijiji cha Ndolezi na Kinyanambo, Kata ya Kinyanambo kwenye moja ya mikutano yake inayoendelea kwa ajili ya kuimarisha chama, alipokuwa akizungumzia juu ya mchakato wa upatikanaji katiba mpya unaoendelea kwenye bunge maalumu la katiba Mjini Dodoma,alisema kwamba Katiba ni njia kuu, Wapingaji ni mchepuko kwani hawaoni kama wajumbe wameshatumia fedha nyingi za watanzania hivyo ni lazima katiba ipatikane.
Mtaturu alisema kwamba katiba sio kitabu cha historia kwamba mtu atasoma na kukiweka ndani, bali katiba ni sheria mama ya Tanzania ambayo ndiyo inayowaongoza watanzania hivyo hakuna haja ya kusimamishwa kwa mchakato huo kwa sababu ya matakwa ya wachache wasiopenda maendeleo katika nchi yenye amani na upendo.
Alisema katiba ndiyo ambayo inataja haki zote za wananchi wa Tanzania, hivyo kama watanzania watakubali kuchezewa na baadhi ya wajumbe wa bunge maalumu la katiba ambao wao wameweka mbele maslahi ya vyama vyao na uroho wa madaraka pasipo kutazama na kuwahurumia wananchi ambao ndio wapiga kura wao na ndio wanaoumizwa kwa kupotea fedha zao nyingi hususani pale ambapo hawatapatiwa katiba, jambo hili litakuwa ni utumwa kimwili na hata kiroho.
Mtaturu alisema katiba ya Tanzania imeandikwa mara tatu, mwaka 1961, 1964 na 1977 baada ya hapo katiba imeandikwa kwa viraka viraka mpaka mwaka 2014 ambapo katiba imeanza kuandikwa tena, ambapo mchakato wa kuandika katiba ulianza tangu mwaka 2012 lakini wapinzani wamekuwa wakipinga kila jambo tangu mchakato huu unaanza hadi hivi sasa.
Hata hivyo katibu alisema kuwa tume ya mabadiliko ya katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Sinde Warioba, ilizunguka nchi nzima kukusanya maoni ambapo hata hivyo ilikusanya maoni kwa watu 356,000 kati ya watanzania 44,000,000 kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.
Alisema pamoja na hayo yote maoni ya watu 200,000 hayakuchambuliwa kwani walichambua maoni ya watu 156,000 pekee.
Alisema watu 37,000 pekee ndio walizungunzia mambo ya muungano na watu 26,000 wanataka serikali tatu, hata hivyo watu 19,000 kati ya watu 26,000 wote wanatoka Mkoa wa Kigoma.
Mtaturu alihoji kama mkoa mmoja wa Kigoma unaweza kuwa na nguvu ya kuamua mustakabali wa taifa la Tanzania lenye jumla ya mikoa 30.
Aliongeza kuwa mfumo wa serikali tatu ni mfumo hatarishi kwa watanzania kwani muarobaini wa maisha ya Mtanzania sio kuwa na serikali 3 ambazo zitaongeza gharama ya matumizi ya fedha za wananchi bali kuwa na serikali mbili zenye mtazamo wa kumsaidia mtanzania kujikomboa katika wimbi zito la umasikini ambalo limejiimarisha hapa nchini Tanzania.
Chanzo:Mjengwa

No comments: