Sunday, July 27, 2014

MUONEKANO WA AJALI YA BAHATI BUKUKU MKOANI DODOMA

Nyota wa nyimbo za Injili Bongo, Bahati Lusako Bukuku ameumia mgongo na maeneo kadhaa ya mwili (nusu kifo) kiasi cha kushindwa kukaa, kusimama wala kutembea kufuatia ajali mbaya ya gari iliyotokea kwenye eneo la Ranchi ya Narco wilayani Kongwa, Dodoma saa tisa usiku wa kuamkia Jumamosi, Ijumaa Wikienda lina undani wa mkasa mzima.

Kwa mujibu wa chanzo makini, katika ajali hiyo ambayo Bahati alikuwa akienda Kahama, Shinyanga kwenye mkutano wa Injili, dereva wa gari alilokuwa akisafiria aina ya Toyota Nadia lenye namba za usajili IT 7945, Edison Mwakabungu ‘Eddy’ (31) aliumia sana kwenye vidole vya miguu na hawezi kutembea.
Muonekano wa gari hilo kwa ubavuni kulia.

Wengine waliokuwemo kwenye ajali hiyo ni wacheza shoo wa Bahati, Frank Muha (20) na mwenzake ambaye jina lake halikupatikana mara moja.
Habari zilidai kuwa gari hilo halikuwa na matatizo hivyo kumfanya dereva wake kukanyaga mafuta kwa wastani wa kilometa 120 kwa saa.“Sasa walipofika eneo la Kibaigwa, walikutana na lori likitokea Dodoma kwenda Morogoro, wakavaana kwa mbele. Nadia likatoka barabarani hadi porini likiwa limeharibika kuanzia kwenye shoo ya mbele, injini na siti za mbele halafu lori hilo likakimbia.

“Nadia ilipotulia, Bahati alijikuta hawezi kufanya chochote, dereva wake naye ameumia kwenye vidole vya miguu. Wale wawili waliokuwa siti ya nyuma, wote walijeruhiwa lakini mmoja si sana. Ilibidi yeye abaki pale na gari ili majeruhi wengine wakimbizwe Hospitali ya Wilaya ya Kongwa, Dodoma kwa matibabu,” kilisema chanzo hicho.
Gari alilopata nalo ajali mwimbaji wa nyimbo za Injili, Bahati Bukuku aina ya Toyota Nadia lenye namba za usajili IT 7945.

No comments:

Zilizosomwa zaidi