Saturday, May 31, 2014

WHO KUONGEZA USHURU WA TUMBAKU ILI KUPUNGUZA WAVUTAJI

Shirika la Afya Duniani WHO limetoa wito wa kuongezwa ushuru tumbaku ili kupunguza uvutaji sigara ambao umebainika kusababisha  vifo ya vya watu milioni sita kila mwaka. 
Katika taarifa iliyotolewa 'Siku ya Kutokuvuta Tumbaku Duniani', WHO imesema hatua za kisera zinahitajika ili kupunguza matumizi ya tumbaku na hivyo kuokoa uhai wa waathirika wa bidhaa hiyo.
WHO inasema kuwa uvutaji tumbaku unaweza kuua zaidi ya watu milioni nane kila mwaka ifikapo mwaka 2030 na hivyo sasa inapendekeza uongezwe ushuru wa bidhaa hiyo . Tayari katika baadhi ya nchi za barani Afrika hatua za kisera zimechukuliwa ili kupunguza ushawishi wa matumizi ya tumbaku kwa binadamu. Takwimu zinaonyesha kuwa ongezeko la kodi kwa asilimia 50 litapunguza wavuta sigara na tumbaku milioni 49 duniani ndani ya miaka mitatu na hivyo kuokoa uhai wa watu milioni 11. WHO imesema kuwa kati ya watu milioni sita ambao hufa kutokana na uvutaji sigara asilimia 80 ni kutoka nchi masikini duniani. Aidha WHO imesema watu laki sita hupoteza maisha kutokana na kuvuta moshi wa wanovuta sigara jambo ambalo linaashiria ulazima wa uvutaji sigara kupigwa marufuku katika maeneo ya umma.

No comments:

Zilizosomwa zaidi