Monday, January 14, 2013

WAKIMBIZI WAISHI KWA MASHAKA AFRIKA MASHARIKI

Hali mbaya kwa wakimbizi katika kambi ya IFO 1 huko Dadaab, karibu na mpaka wa Kenya na Somalia.
wakimbizi wanaeleza kwamba wanalazimika kuhama kambi kutokana na ukosefu wa huduma za msingi, unyanyasaji, uhalifu, ubakaji na hakuna mfumo wa elimu kwa watoto wanaoishi kwa muda mwingi ndani ya kambi.
Kenya hivi karibuni iliwaamrisha wakimbizi wote walohama katika miji mbali mbali kurudi katika kambi ya Dadaab, kambi kuu ya wakimbizi barani Afrika, hiyo ikiwa njia moja ya kujibu wimbi la masham bulizi ya kigaidi katika miji ya nchi hiyo.

No comments:

Zilizosomwa zaidi