Wednesday, December 26, 2012

HUU NDIO UJUMBE WA PAPA BENEDICT WA 16 KWENYE TWITTRER

 


Papa akituma ujumbe wake wa Twitter
Papa Benedict wa 16 ametuma ujumbe wake wa kwanza kwenye akaunti yake yaTwitter. Ujumbe huu ulikuwa umesubiriwa kwa hamu sana.
Alionekana akibonyeza kwenye tabiti yake ya iPad na kutuma ujumbe huo
UJumbe wake ulikuwa unasoma hivi ''Marafiki wapendwa, nimefurahi sana kuwasiliana nanyi kupitia Twitter. Asanteni sana kwa ujumbe wenu na ninawabariki nyote.''
Msemaji wake alisema kuwa ujumbe wa Papa utafikia kila mtu amjuaye kwa kutumia akaunti zake zilizo kwenye lugha saba.

Akaunti ya papa iliyo kwenye lugha ya kiingereza tayari ina wafuasi zaidi ya laki sita.
Akaunti zake zote ambazo ni @pontifex zinafuatana moja baada ya nyingine.
Mwaka jana Papa alituma ujumbe wake wa kwanza kutoka Vatican kuweza kuzindua mtandao wake wa maelezo mbali mbali.
Papa ni kiongozi wa waumuni bilioni 1.2 wa kikatoliki na atakuwa akitia saini ujumbe wake wala hatoundika mwenyewe.

No comments:

Zilizosomwa zaidi