(PICHA ZOTE NA Faraja Dogeje)
Tuesday, May 21, 2013
VODACOM WADAI KUWA ULE UJUMBE WA VITISHO ALIOTUMIWA LEMA HAUKUTOKA KWA MKUU WA MKOA ..
Kamanda wa Polisi Mkoani wa Arusha, Liberatus Sabas, amedai kuwa uchunguzi wa
awali kuhusu ujumbe unaodaiwa kutumwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa
Mulongo, umetumwa na mtandao wa simu wa nje ya nchi.
Kamanda alisema katika ujumbe huo ambao Lema anadai uliandikwa na Mkuu wa Mkoa Mulongo na kutumwa kwenye simu yake Aprili mwaka huu, uchunguzi wa polisi umeonyesha kwamba haukutumwa kupitia kampuni moja wapo ya simu za mikononi ya hapa nchini.
“Katika kipindi cha mwishoni mwa Aprili mwaka huu, vyombo vingi vya habari vikiwemo radio, magazeti na mitandao ya kijamii viliandika na kutangaza habari iliyoelezea shutuma zilizotolewa na Mbunge Lema kuwa aliandikiwa ujumbe wa vitisho kwa njia ya simu na Mkuu wa Mkoa Mulongo na ulisomeka:
“Umeruka kihunzi cha kwanza nitakuonyesha mimi ni serikali, ulikojificha nitakupata na nitakupa kesi inayoitaka mimi.”
Kamanda Sabas alisema ujumbe huo ulidaiwa kutumwa kutoka namba 0752960276 inayotumiwa na Mkuu wa Mkoa Mulongo kwenda kwenye namba 0764150747 inayotumiwa na Lema. Alisema kufuatia tuhuma hizo, polisi walianza uchunguzi kwa kuzingatia kuwa Mulongo alikanusha kutuma ujumbe wa aina yo yote kwa Mh Lema.
Alisema uchunguzi huo ulihusisha kampuni ya simu ambayo mtandao wake ulitumika katika utumaji wa ujumbe husika. Alisema uchunguzi wa awali wa polisi umebaini kuwa chanzo cha ujumbe huo mfupi hakikuwa kampuni ya simu husika (hakuitaja) kwa vile ‘Centre Number’ iliyotumika kutuma ujumbe huo mfupi wa maneno ni 44780200332, ambayo siyo ya mtandao wa kampuni husika bali ni ya mtandao ulio nje ya nchi.
Alisema uchunguzi zaidi unaendelea kubaini chanzo cha ujumbe huo mfupi wa simu na mtu aliyehusika kutuma hatua za kisheria zitaweza kuchukua mkondo wake.
Kamanda alisema katika ujumbe huo ambao Lema anadai uliandikwa na Mkuu wa Mkoa Mulongo na kutumwa kwenye simu yake Aprili mwaka huu, uchunguzi wa polisi umeonyesha kwamba haukutumwa kupitia kampuni moja wapo ya simu za mikononi ya hapa nchini.
“Katika kipindi cha mwishoni mwa Aprili mwaka huu, vyombo vingi vya habari vikiwemo radio, magazeti na mitandao ya kijamii viliandika na kutangaza habari iliyoelezea shutuma zilizotolewa na Mbunge Lema kuwa aliandikiwa ujumbe wa vitisho kwa njia ya simu na Mkuu wa Mkoa Mulongo na ulisomeka:
“Umeruka kihunzi cha kwanza nitakuonyesha mimi ni serikali, ulikojificha nitakupata na nitakupa kesi inayoitaka mimi.”
Kamanda Sabas alisema ujumbe huo ulidaiwa kutumwa kutoka namba 0752960276 inayotumiwa na Mkuu wa Mkoa Mulongo kwenda kwenye namba 0764150747 inayotumiwa na Lema. Alisema kufuatia tuhuma hizo, polisi walianza uchunguzi kwa kuzingatia kuwa Mulongo alikanusha kutuma ujumbe wa aina yo yote kwa Mh Lema.
Alisema uchunguzi huo ulihusisha kampuni ya simu ambayo mtandao wake ulitumika katika utumaji wa ujumbe husika. Alisema uchunguzi wa awali wa polisi umebaini kuwa chanzo cha ujumbe huo mfupi hakikuwa kampuni ya simu husika (hakuitaja) kwa vile ‘Centre Number’ iliyotumika kutuma ujumbe huo mfupi wa maneno ni 44780200332, ambayo siyo ya mtandao wa kampuni husika bali ni ya mtandao ulio nje ya nchi.
Alisema uchunguzi zaidi unaendelea kubaini chanzo cha ujumbe huo mfupi wa simu na mtu aliyehusika kutuma hatua za kisheria zitaweza kuchukua mkondo wake.
BARUA TOKA VODACOM
ISOME HAPA STORI YA MAJAMBAZI WALIOANGUSHA MFUKO WENYE MAMILIONI YA PESA KWENYE ENEO LA MAKABURI JIJINI DAR
Katika tukio hilo lililotokea saa tisa usiku, Polisi walipiga risasi juu baada ya kupewa taarifa na majirani, na kuwafanya majambazi hao waliokuwa tisa, kutimua mbio kwa kuruka ukuta upande wa makaburini na kuangusha mfuko wenye fedha zaidi ya Sh milioni tatu, fedha za kigeni na simu mbili.
Paroko wa kanisa hilo, Padri Mathew Chavely alimwambia mwandishi jana kuwa, majambazi hao walivunja mlango wa ofisi baada ya kuwafunga kamba walinzi na kuwawekea plasta midomoni kisha kufanikiwa kuiba fedha hizo.
“Tulijua wakitoka ofisini, wanatujia sisi nyumbani, ila kabla, watu wema walitoa taarifa polisi na mara polisi wakaja hapa, walipiga risasi wale wezi wakakimbia na fedha zote, asubuhi wakati wa uchunguzi, kumbe waliangusha fedha makaburini, karibu na kanisa,” alisema Padri Chavely.
Alipoulizwa kwa nini wakae na fedha nyingi ofisini, Padri Chavely alisema kanisani hapo hivi sasa wanaendelea na ujenzi wa kanisa jipya kubwa, hivyo Jumapili ya juzi, mbali ya kukusanya sadaka za kawaida, kulikuwa na harambee ya ujenzi wa kanisa hilo.
Padri Chavely aliwashukuru waumini na majirani kwa sala na kutoa taarifa polisi na aliwaombea majambazi hao wabadilike, wamrudie Mungu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Ulrich Matei alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa, asubuhi walimshikilia Karani wa Ofisi, Deus Cosmas kwa mahojiano, lakini walimuachia baada ya kupata simu mbili za majambazi hao zilizodondoshwa makaburini pamoja na fedha zote.
“Ni kweli saa tisa usiku leo (jana) walivamia kanisa hilo, wezi waliokuwa tisa, wakiwa na silaha za jadi kama marungu, mapanga, nyundo na nyinginezo, tulipopata taarifa tulifika mara moja na kwa kuwa hatukujua walioko ndani wana silaha gani zaidi, tuliamua kupiga risasi juu, ndipo walipokimbia kwa kuruka ukuta nyuma, eneo la makaburini,” alisema Kamanda Matei.
Akielezea zaidi tukio hilo, Kamanda Matei alisema wezi hao waliwafunga kamba na plasta walinzi kabla ya kuvunja ofisi ya kanisa na kuiba Sh 3,172,450, Dola za Marekani 13, fedha za Uganda Sh 18,700, fedha za Kenya Sh 200 na Rupia 328.
Kwa mujibu wa Polisi, kutokana na ukubwa wa eneo hilo, majambazi walitumia ukuta wa nyuma kuruka na kukimbia na wakati wakikimbia, katika eneo hilo lenye makaburi, walikuta damu kwenye misalaba kadhaa iliyoharibiwa kwa kupindishwa na kutokana na purukushani hiyo, waliangusha mfuko wenye fedha zote walizoiba na simu hizo mbili.
Kamanda Matei alisema usalama umeimarishwa eneo hilo, na kupitia simu hizo, kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), wamebaini mtandao na mambo mengi ambayo yatawawezesha kuwakamata wote wanaohusika na tukio hilo na matukio mengine mkoani humo.
LISSU AENDELEA KUMWAGA SERA KWA WANANCHI WA SINGIDA..

Mbunge wa jimbo la Singida mashariki Mh. Tundu Lissu akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni ya nafasi ya udiwani kata ya Iseke tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi uliofanyika katika kijiji cha Iseke.


Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Iseke tarafa ya Ihanja waliohudhuria uzinduzi wa kampeni ya udiwani kata ya Iseke uliofanywa na chama cha CHADEMA.

Baadhi ya viongozi wa CHADEMA waliohudhuria uzinduzi wa kampeni ya udiwani wa kata ya Iseke tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi.(Picha zote na Nathaniel Limu).
Mgeni rasmi katika kampeni ya uzinduzi wa nafasi ya udiwani kata ya Iseke tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi Mh. Tundu Lissu, ameashindwa kuuza sera za CHADEMA na badala yake ametumia muda na nguvu nyingi kuhimiza sera yake ya ‘katazo’ la wananchi kuchangia maendeleo yao .
Mh. Tundu Lissu ambaye ni mbunge wa jimbo la Singida Mashariki kupitia tiketi ya CHADEMA, alipanda jukwaani huku akiwa mabeba makabrasha ya michanganuo ya bajeti ya serikali ya kuanzia mwaka wa fedha wa 2010/2011 hadi 2013/2014.
Akisema na kushangiliwa kwa nguvu na wananchi waliohudhuria uzinduzi huo uliofanyika katika kijiji cha iseke, Mh Tundu Lissu aliweka wazi kuwa “Mimi sitaki kabisa kuzungumzia habari za Amosi Mghenyi ambaye ametusaliti kwa kuhama CHADEMA na kurejea CCM. Amosi kisiasa ni mfu, kwa hiyo siwezi kupoteza muda wangu kuzungumiza mambo ya mfu”.
Amesema ufunguzi wake utajikita zaidi katika kuwaelimisha wananchi wa kata ya Iseke kwamba serikali inayo fedha nyingi na za kutosha kugharamia maendeleo ya wananchi.
Akiijengea nguvu hoja yake hiyo, amesema kwa mfano katika mwaka wa fedha wa 2010/2011, mkoa wa Singida, ulipewa zaidi ya shilingi milioni 903 za undeshaji wa shule, lakini zilizotumika ni zaidi ya shilingi milioni 464 na kubaki zaidi ya shilingi 438.2.
Amesema fedha hizo zaidi ya shilingi 438.2 zilizobaki, hazijaainishwa zilipelekwa wapi. “Kwa vyo vyote zitakuwa zimeishia kwenye matumbo ya mgambo na watendaji wa serikali ya CCM”.
Mh. Tundu ambaye pia ni mwanasheria kitaaluma, amewataka wakazi wa kata ya Iseke, kumchagua Emmnuel Jackson Jingu awe diwani wao, ili waondokane na manyanyaso ya michango kama walivyojikomboa wakazi wa jimbo la Singida Mashariki.
Wagombea wengine wa nafasi ya udiwani kata ya Iseke ni Amosi Munghenyi wa CCM na Abdallah Kinyenje maarufu kwa jina la Petro wa CUF.
CHANZO MO BLOG
Subscribe to:
Posts (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
Israel Magesa Wakili Magesa aliyeko (pichani) amefariki dunia ghafla leo asubuhi. Wakili Magesa, ambaye ni mmiliki wa kampuni y...
-
GARI aina ya Toyota VX linaloelezwa kuwa mali ya Serikali limekamatwa na polisi likiwa limebeba pembe za ndovu. ...
-
-
Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemkamata mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji likimtuhumu kuchochea vurugu za kupinga mradi wa bo...
-
Nimepokea mwaliko wa kikao maalumu cha kikao cha fedha na uongozi wa tarehe 3/01/2014 kikao kufanyika tarehe 06/01/2013 saa nane mchana ...



